Waadventista wasabato huipokea Biblia kama
kanuni yao pekee na hushika baadhi ya
misingi ya imani kuwa ndiyo mafundisho ya
mabadiliko matakatifu . Imani hizi , kama
zilivyoorodheshwa hapa , hufanya welekevu
wa kanisa na udhihirisho wa mafundisho ya
mabadiliko. Masahihisho ya kauli hizi
yanaweza kutegemewa katika kikao cha
Halmashauri
kuu wakati kanisa likiongozwa na Roho
Mtakatifu kwenye ufahamu ulio kamili zaidi
ya
ukweli wa Biblia au linapopata lugha iliyo
bora zaidi ya kuelezea mafundisho ya Neno
Takatifu la Mungu.
1. Maandiliko Matakatifu
Maandiko Matakatifu , yaani Agano la kale na
Jipya ndiyo Neno la Mungu lililoandikwa,
likatolewa kwa uvuvio wa Mungu, kupitia
kwa watu watakatifu walionena na kuandika
kama
walivyoagizwa na Roho Mtakatifu. Ndani ya
neno hili , Mungu amemkabidhi mwanadamu
maarifa yaliyo lazima kwa ajili ya wokovu.
Maandiko matakatifu ni ufunuo usioweza
kukosa
wa mapenzi yake . Ndiyo upeo wa tabia ,
kipimo cha uzoefu , ufunuo thabiti wenye
mamlaka
wa mafundisho ya imani, na kumbukumbu
aminifu ya matendo ya mungu katika historia.
( 2 Petro 1 : 20 ,21 . 2 Timotheo 3: 16 , 17 . Zaburi
119: 105. Mithal 30 : 5, 6. Isaya 8: 20 . Yoh
17 : 17 . 1Wathe 2: 13 . Waeb 4 : 12 . )
2. Utatu Mtakatifu
Kuna Mungu mmoja : Baba , Mwana, na Roho
Mtakatifu, umoja wa nafsi tatu za milele.
Mungu hapatikani na mauti , mwenye nguvu
zote , ajuaye yote, zaidi ya yote, na aliyeko
daima . Yeye hana mwisho na ni zaidi ya
ufahamu wa kibinadamu , hata hivyo
anafahamika
kupitia kujifunua kwake binafsi . Milele zote
yu astahili kuabudiwa , kusujudiwa ,
kutumikiwa
na viumbe vyote . ( kumb 6 : 4 . Mith 28 : 19 . 2 kor
13 : 14 . Waef 4 : 4 -6 . 1Petr 1 : 2 1 Tim 1: 17
Ufunuo 14 : 7 )
3. Baba
Mungu Baba wa milele ndiye muumbaji ,
Chimbuko , Mtengenezaji , na Mfalme wa
viumbe
wote . Ni mwenye haki na Mtakatifu , Mwingi
wa rehema ,, mwenye fadhili , si mwepesi wa
hasira, na mwingi wa uthabiti wa upendo na
uaminifu . Tabia na uwezo vilivyodhihirishwa
ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni
ufunuo wa Baba . ( Mwanzo 1 : 1 Ufu 4: 11 .
1wakor 15 : 28 . Yoh 3 : 16 . 1 Yoh 4: 8. 1 Tim 1: 17 .
Kut 34 : 6 ,7 . Yoh 14 : 9) .
4. Mwana
Mungu Mwana wa milele alifanya mwili
katika Yesu Kristo. Kupitia kwake vitu vyote
viliumbwa , tabia ya mungu imefunuliwa ,
wokovu wa wanadamu unakaribishwa na
ulimwengu unahukumiwa . Milele zote Mungu
kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu
aliye kristo. Alichukuliwa mimba kwa uwezo
wa Roho Mtakatifu na kuzaliwa na bikira
Mariamu . Akaishi na kupitia uzoefu majaribu
kama mwanadamu , lakini kwa ukamilifu
alioonyesha kwa mfano wa haki na u [ endo
wa Mungu. Kwa miujiza yake alidhihirisha
uwezo wa Mungu na alithibitishwa kama
Masihi aliyeahidiwa. Aliteseka na kufa kwa
hiari
msalabani kwa ajili ya dhambi zetu , na kama
mbadala wetu , Alifufuliwa kutoka kwa wafu ,
na akapaa kuhudumu katika hekalu la
mbinguni kwa niaba yetu. Atakuja tena katika
utukufukwa ajili ya ukombozi wa mwisho wa
watu wake na urejeshwaji wa vitu vyote . ( Yoh
1: 1 -3 ,14 . Wakol 1: 15 - 19 , . Wafil 2 : 5 -11 . Yoh
10 : 30 , 14 : 9 Warum 6 : 23 . 2Wakor 5: 17 -19 .
Yoh 5 : 22 . 1Wakor 15 : 3 ,4 . Luka 1 : 35 . Yoh
14 : 1 - 3)
5. Roho Mtakatifu
Mungu Roho wa milele alikuwa mtendaji
pamoja na Baba na Mwana katika uumbaji ,
kufanyika mwili , na katika ukombozi .
Aliwavuvia waandishi wa mabadiliko
matakatifu .
Alijaza maisha ya kristo na uwezo . Huwavuta
na kuwasadikisha wanadamu , na wale
wanaoitikia huwafanya upya na
kuwabadilisha katika sura ya Mungu.
Akipelekwa na Baba
na Mwana ili kuwa siku zote pamoja na
watoto wake, hutoa karama za kiroho kwa
kanisa ,
huliwezesha kumshuhudia kristo, na kwa
upatano wa maandiko uliongoza kwenye
ukweli
wote . ( Mwa 1 ,2 . Luka 1: 35 , 4 : 18 . Mdo 10 : 38 .
2Petr 1 : 21 . 2 Wakor 3 : 18 . Yoh 14 : 16 -18 , 26 ,
15 : 26 ,27 , 16 : 7 -13 )
6. Uumbaji
Mungu ni muumba wa vitu vyote , na
amefunua katika maandiko uhalisi wa tukio
la
shughuli zake za uumbaji . Katika siku sita
Bwana alizifanya “ Mbingu na Nchi ” na vitu
vyote
vilivyoko hai juu ya nchi, akastarehe siku ya
saba ya juma lile la kwanza . Na hivyo
akaanzisha sabato kama kumbukumbu ya
milele ya kukamilika kwa kazi yake ya
uumbaji.
Mwanaume na Mwanamke wa kwanza
walifanywa kwa mfano wa Mungu kama upeo
wa
kazi yake ya Uumbaji , wakapewa utawala juu
ya ulimwengu , na wakaagizwa kuajibika na
utunzaji wake. Wakati ulimwengu
ulipomalizika kila kitu kilikuwa “ ni chema
sana ”
ukitangaza utukufu wa Mungu. ( Mwa 1 ,2 .
Kut20 : 8 - 11 . Zab 19 : 1 -6 , 33 : 6 -9 , 104. Waebr
11 : 3 )
7. Asili ya Mwanadamu
Mwanaume na Mwanamke walifanyawa kwa
mfano wa Munguwakiwa kila mmoja na nafsi
yake, uwezo na uhuru wa kufikirina kutenda .
Ingawa waliumbwa viumbe huru , kila mmoja
ni umoja wa nafsi isiyogawanyika ya mwili ,
akili na roho, akimtegemea Mungu kwa uhai
na
pumzi na mengine yote. Wakati wazazi wetu
wa kwanza walipomwasi Mungu, walikana
utegemezi wao kwa Mungu na wakaanguka
kutoka hadhi yao ya juuchini ya Mungu. Sura
ya Mungu iliyopo ndani yao ikaharibika na
wakawa chini ya mauti . Wazao wao hushiriki
asili hii ya kuanguka na matokeo yake.
Wanazaliwa wakiwa na udhaifu na mivuto ya
kuelekea kwenye uovu . Lakini Mungu katika
kristo aliupatanisha ulimwengu na nafsi yake ,
na kwa Roho wake hurejesha ndani ya
mwanadamuwatubuo sura ya muumba wao .
Wakiwa wameumbwa kwa ajili ya utukufu
wa Mungu, wanaitwa kumpenda na
kupendana
wao kwa wao na kutunza mazingira yao.
( Mwa 1 : 26 -28 , 2 : 7 . Zab 8 : 4- 8. Mdo 17 : 24 - 28 .
Mwa
3. Zab 51 : 5 War 5 : 12 : 17 . 1Yoh 4 : 7 ,8 ,11 , 20 .
Mwa 2 : 15
8. Pambano kuu
Jamii yote ya wanadamu sasa inahusika
katika pambano kuu baina ya kristo na
shetani
kuhusu tabia ya Mungu, sheria yake , na
utawala wake juu ya ulimwengu . Ugomvi huu
ulianza mbinguni wakati kiumbe aliyeumbwa
na kutunukiwa uhuru wa kuchagua , katika
kujiinua akawa shetani , mpinzani wa Mungu,
na kupelekea sehemu ya Malaika kwenye
uasi . Akaiagiza Roho ya uasi katika
ulimwengu huu pale alipowaongoza Adamu
na Hawa
kingia dhambini. Dhambi hii ya mwanadamu
ilileta matokeo ya upotoshaji ya sura ya
Mungukatika wanadamu , Uvurugaji wa
ulimwengu ulioumbwa , na mwishowe
kuteketea
wakati wa gharika iliyokumba ulimwengu
wote . Ukitazamwa na viumbe wote
ulimwengu
huu ukawa uwanja wa vita ya ulimwengu,
ambao kutokana nao Mungu wa upendo
hatimaye akathibitika kuwa mwenye haki .
Katika kuwasaidia watu wake katika pambano
hili , kristo anamtuma Roho Mtakatifu na
malaika watiifu kuongoza , kulinda , na
kutegemeza katika njia ya wokovu . ( Ufu
12 : 4 - 9, Isa 14 : 12 - 14 , Eze 28 : 12 - 18 , War
1: 19 - 32 ,
5: 12 - 21 , 8: 19 - 22 , 1Wakor 4: 9, Waeb 1 : 14 )
9. Maisha, Mauti na Ufufuo wa kristo
Katika maisha ya kristo ya utii mtakatifu kwa
mapenzi ya Mungu, mateso yake , mauti na
ufufuo , Mungu alitoa njia pekee ya kafara
kwa ajili ya dhambi ya mwanadamu , ili
kwamba
wale ambao kwa imani wanapokea
upatanisho huu waweza kuwa na uzima wa
milele, na
ulimwengu wote uweze kuelewa vizuri
upendo mtakatifu usio na kikomo wa
muumba.
Kafara hii kamilifu huthibitisha haki ya
sheria ya mungu na fadhili za tabia yake , kwa
sababu hufanya vyote viwili kuhukumu
dhambi zetu na kutupatia msamaha . Kifo cha
kristo
ni cha badala na cha kulipia, kupatanisha na
chenye kubadilisha . Ufufuo wa Yesu kristo
hutangaza ushindi wa Mungu dhidi ya nguvu
za uovu , na kwa wale wanaopokea kafara
huakikisha ushindi wao wa mwisho dhidi ya
dhambi na mauti . Kinatangaza ukuu wa Yesu
Kristo, ambaye mbele zake kila goti mbinguni
na duniani litapigwa . ( Yoh 3 : 16 , Isa 13 : 1,
1Petr 2 : 21 , 22 ,1 Wakor 15 : 3 , 4 , 20 -22 , 2Wakor
5: 14 , 19 - 21 . War1 : 4 , 3 : 25 , 4 : 25 , 8 : 3 , 4,
Wafil2: 6 -11 )
10 . Uzoefu wa Wokovu
Katika upendo usio na mwisho na rehema
zake Mungu alimfanya Kristo , asiyejua
dhamdi
kuwa dhambi kwa ajili yetu , ili kwambakatika
yeye tuweze kufanywa haki ya Mungu.
Tukiongozwa na Roho mtakatifu tunatambua
hitaji letu, tunakili hali yetu ya kuwa wenye
dhambi , tunatubu maasi yetu , na kuonyesha
imani katika Yesu kama Bwana na Kristo ,
kama mbadala na kielelezo. Imani hii
inayopokea wokovu huja kupitia katika uwezo
wa
kimbingu wan a ni karama ya neema ya
Mungu. Kupitia kwa kristo tunahesabiwa
haki ,
tunafanywa kuwa wana wa binti za Mungu,
na kukomesabiwa haki kutoka katika hali ya
kuwa chini ya dhambi . Kupitia kwa Roho
tunazaliwa upyana kutakaswa , Roho
hufanywa
upya nia zetu , huandika sheria ya Mungu ya
upendo katika mioyo yetu , na tunapewa
uwezo
wa kuishi maisha matakatifu . Tukikaa ndani
yake tunakuwa washiriki wa asili ya uungu
na
tuna hakika ya wokovu sasa na katika
hukumu . ( 2 Wakor 5 : 17 - 21 , Yoh 3 : 16 , Wag 1 : 4 ,
4: 4-
7, Tito3 : 3 -7 , Yoh 16 : 8 , Wag 3 : 13 , 14 . 1 Petr
2: 21 ,22 . Warumi 10 : 17 , 3 : 21 -26 , 8 : 14 -17 , 12 : 2 .
Warumi 8 : 1- 4, 5: 6- 10 , 2 Petr 1 : 3, 4)
11 . Kukua katika kristo
Kwa kifo chake msalabani Yesu alizishinda
nguvu za uovu . Yeye aliyewatiisha pepo
wachafu wakati wa huduma yake hapa
duniani amezivunja nguvu zao na
kuthibitisha
mwisho wao ni uangamivu usioepukika .
Ushindi wa Yesu utupatia ushindi dhidi ya
nguvu
za uovu ambazo bado zinatafuta kututawala ,
tunapo tembea naye kwa amani, fyraha , na
uhakika wa upendo wake. Sasa Roho Mtakatifu
anakaa ndani yetu na kututia nguvu .
Tukidumu kujikabidhi kwa Yesu kama Bwana
na mwokozi wa maisha yetu tunawekwa
huru kutoka katika mzigo wa matendo yetu
yaliyopita . Hatuishi tena gizani , katika hofu
ya
nguvu za uovu , ujinga , na katika kukosa
maana kwa namna ya maisha yetu ya awali, .
Katika
uhuru huu mpya ndani ya kristo, tumeitwa
kukua katika kufanana na tabia yake ,
tukiongea
naye kila siku katika sala , na kujilisha neno
lake kikamilifu , tukikusanyika pamoja kwa
ajili
ya ibada , na kushiriki katika utume wa
kanisa . Tukijitoa katika kuwahudumia kwa
upendo
wale wanaotuzunguka na kuwashuhudia
wokovu wake, kuwepo kwake nasi daima kwa
njia
ya Roho hugeuza kila wasaa na kazi kuwa
uzoefu wa kiroho . ( Zab. 1: 1, 2. 23 : 4 , 77 : 11 ,12 ,
Kol 1: 13 -14 , 2: 6, 14 - 15 , Luka 10 : 17 -20 ,
Efe5 : 19 -20 , 6 : 12 -18 , 1 Theo 5 : 23 , 2Petr 2 : 9 ,
3: 18 .
Fil3 : 7 -14 , Math 20 : 25 -28 , Yoh 20 : 21 ,
Gal 5: 22 - 25 , Rum 8 : 38 - 39 , 1Yoh 4: 4, Ebr10
12 . Kanisa
Kanisa ni jamii ya waumini wanaomkiri Yesu
kristo kuwa bwana na mwokozi katika
mfululizo wa kufungamana na watu wa
Mungu katika nyakati za agano la kale,
tunaitwa
kutoka katika ulimwengu, na tunajiunga
pamoja kwa ajili ya ibada , kwa ajili ya
ushirika, kwa
ajili ya mafundisho katika neno , na kwa ajili
ya maadhimisho ya meza ya bwana , kwa ajili
ya
huduma kwa wanadamu wote , na kwa ajili ya
tangazo la injili ulimwenguni kote , kanisa
linapata mamlaka yake kutoka kwa kristo,
aliye neno lililofanyika mwili , na kutoka
katika
maandiko, ambayo ndiyo neno lililoandikwa.
Kanisa ni jamaa ya Mungu, waliofanywa nay
eye kuwa watoto wake, washiriki wake huishi
katika misingi ya agano jipya . Kanisa ni mwili
wa Kristo, jamii ya weny imani ambayo kristo
mwenyewe ndiye kichwa. Kanisa ni bibi arusi
ambaye kwa ajili yake kristo apate kulisafisha
na kulitakasa . Wakati wa kurudi kwake kwa
ushindi, ataliwasilisha kwake mwenyewew
kanisa lenye utukufu , waaminifu wa karne
zote ,
walionunuliwa kwa damu yake , lisilo na waa
au kunyanzi , lakini takatifu na lisilo na
ila . ( Mwa 12 : 3, Mdo : 7 : 38 , Waef 4 : 11 -15 , 3 : 8 -11 ,
Math 28 : 19 ,20 , 16 : 13 - 20 , 18 : 18 ,
Waef 19 : 22 ,23 , 5 : 23 -27 , Wakol 1 : 17 - 18 ) .
13 . Masalio na Utume Wake
Kanisa la ulimwengu lijumuisha wale wote
ambao kwa kweli wanamwamini kristo, lakini
katika siku za mwisho , kipindi cha kuenea
kwa ukengeufu , masalio wameitwa kuzishika
amri za Mungu na imani ya Yesu kristo .
Masalio hawa hutangaza kuwadia kwa saa ya
hukumu , hutangaza wokovu kupitia kristo, na
hupiga mbiu ya kukarinia kwa marejeo yake .
Tangazo hili huwakilishwa katika mfano wa
malaika watatu wa ufunuo 14 , juambatana na
kazi ya hukumu mbinguni na kuwa na
matokeo ya kazi ya toba na matengenezo
duniani .
Kila muumini anatakiwa kuwa na sehemu
binafsi katika ushuhuda huu wa ulimwenguni
kote . ( Ufu 12 : 17 , 14 : 6 -12 , 18 : 1 -4 , 2Wakor 5: 10 ,
Yuda 3, 14 , 1Petro1 : 16 -19 , 3 : 10 -14 ,
Ufu 21 : 1- 14 )
14 . Umoja katika Mwili wa Kristo
Kanisa ni mwili mmoja ulio na washiriki
wengi, walioitwa kutoka katika taifa , kabila ,
lugha,
na watu. Katika kristo tu viumbe wapya ,
ubainishi wa rangi, tamaduni , elimu , na taifa ,
na tofauti kati ya tabaka ya juu nay a chini ,
tajiri na maskini , mwanaume na
mwanamke , havipaswi kuleta mgawanyiko
miongoni mwetu . Sote tu sawa katika kristo,
ambaye kwa roho mmoja ametufunga katika
ushirika mmoja pamoja nay eye na sisi
wenyewe kwa wenyewe, tunapaswa kutumika
na kutumikiwa pasipo kupendelea au kusita.
Kupitia kwa Yesu kristo katika maandiko
tunashiriki imani na tumaini moja , na
tunawafikia
wote kwa ushuhuda mmoja . Umoja huu una
chimbuko lake katika umoja wa Mungu
mmoja mwenye nafsi tatu , ambaye
ametufanya sisi tu watoto wake. ( War12 : 4 ,5 ,
1Wakor 12 : 12 - 14 , Math 28 : 19 ,20 , Zabr133: 1,
2Wakor 5 : 16 ,17 , Mdo 17 : 26 ,27 , Waef 4 : 14 -16 ,
4: 1- 6 , Yoh 17 : 20 -23 )
15 . Ubatizo
Kwa njia ya ubatizo tunakiri imani yetu
katika kifo na ufufuo wa Yesu kristo, na
kushuhudia kufia kwetu dhambi na kusudi
letu la kuenenda katika upya wa maisha.
Hivyo
tunamkubali kristo kuwa Bwana na Mwokozi ,
tunakuwa watu wake, na tunapokelewa kama
washiriki wa kanisa lake. Ubatizo ni mfano
wa muungano wetu na kristo , msamaha wa
dhambi zetu na kupokea kwetu Roho
Mtakatifu. Ni kwa kuzamishwa najini na
unategemea
uthibitisho wa imani katika yesu na ushindi
wa toba ya dhambi . Unafuata mafunzo katika
maandiko matakatifu na ukubali wa
mafundisho yake . ( Warum 6 : 1 -6 ,
Wakol2 : 12 ,13 ,
Mdo16 : 30 - 33 , 22 : 16 , 2: 38 , Math 28 : 19 -20 )
16 . Meza ya Bwana
Meza ya Bwana ni ushiriki katika mfano wa
mwili na damu ya Yesu kama udhihirisho wa
imani katika yeye , Bwana na mwokozi wetu .
Katika ushirika huu kristo anakuwepo
kukutana na kuwaimarisha watu wake. Kadri
tunavyoshiriki , kwa furaha tunatangaza mauti
ya Bwana mpaka arudipo tena. Maandalizi
kwa ajili ya meza ya Bwana hujumuisha
kujihoji
nafsi, toba na ungamo . Bwana aliamua
huduma ya kutawadhana miguu kumaanisha
kutakaswa upya , kuonyesha nia ya
kutumiana wenyewe kwa wenyewe katika
unyenyekevu
ufananao na wa kristo , na kuungana mioyo
yetu katika upendo . Huduma ya Meza ya
Bwana wazi kwa waumini wote wakristo .
( 1 Wakor 10 : 16 ,17 . 11 : 23 -30 , Math 26 : 17 -30 ,
Ufu 3: 20 , Yoh 6 : 48 -63 , 13 : 1 -17 )
17 . Karamu za Roho na Huduma
Mungu huwakirimia washiriki wote wa kanisa
lake katika kila kizazi karama za kiroho
ambazo kila mshiriki atatumia katika huduma
ya upendo kwa ajili ya mema ya kawaida ya
kanisa na wanadamu . Zikitolewa kwa wakala
wa Roho Mtakatifu , ambaye humgawia kila
mshiriki kama apendavyo yeye , karama hizo
hutoa uwezo wote na huduma zinazohitajiwa
na kanisa katika kuytekeleza shughuli zake
zilizoamuriwa na Mungu. Kulingana na
maandiko huduma hizi hujumuisha huduma
kama : Imani , uponyaji, unabii , mahubiri ,
mafundisho, utawala , upatanisho , huruma , na
huduma ya kujinyima na ufadhili kwa ajili ya
msaada na faraja kwa watu . Baadhi ya
washiriki huitwa na mungu na kukirimiwa na
Roho
kwa ajili ya shughuli zinazotambuliwa na
kanisa katika uchungaji , uinjilisti , na utume,
na
huduma za kufundisha zinahitajika hasa
katika kuwapatia zana washiriki kwa ajili ya
huduma kulijenga kanisa hadi ukomavu wa
kiroho, na kukuza umoja wa imani na
maarifa
ya Mungu. Pale washiriki wanapozitumia
karama hizi za kiroho kama mawakili
waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu,
kanisa hulindwa dhidi ya mivuto miharibifu
ya
mafundisho ya uwongo, na hukua kwa ukuaji
unaotoka kwa Mungu, nakujengeka imara
katika imani na upendo . ( Warumi 12 : 4 -8 ,
1Wakor 12 : 9 -11 , 27 ,28 . Waef 4 : 8 ,11 , Mdo 6 : 1 -7 ,
1Petr 4: 10 - 11 )
18 . Karama ya Unabii
Mojawapo ya karama za Roho Mtakatifu ni
unabii, karama hii ni alama -kitambulisho cha
kanisa la masalio na ilidhihirishwa katika
huduma ya Ellen G . White . Kama mjumbe wa
Bwana , maandishi yake ni chanzo kiendelezi
na yenye mamlaka ya ukweli yanayolipatia
kanisa faraja, uongozi, mafundisho , na
maonyo . Pia yanaweka wazi kuwa Biblia
ndiyo
kanuni ambayo kwa hayo mafundisho yote na
uzoefu lazima vipimwe . ( Yoeli 2 : 28 ,29 ,
Mdo2 : 14 -21 , Waeb 1 : 1- 3, Ufu 12 : 17 , 19 : 10 )
19 . Sheria ya Mungu
Kanuni kuu za sheria ya Mungu zimetiwa
pamoja katika Amri kumi na mfano wake
ulidhihirishwa katika maisha ya kristo,. Nazo
zinadhihirisha upendo wa Mungu, mapenzi
yake, na makusudi yake kuhusu mwenendo
wa binadamu na mahusiano nazo ni sharti
kwa
watu wote katika kila kizazi. Amri hizi ndiyo
msingi wa agano la Mungu na watu wake na
kanuni katika hukumu ya Mungu. Kupitia
uwakala wa Roho Mtakatifu zinasonda
dhambi
na kuhamsha hisia za hitaji la mwokozi .
Wokovu wote ni katika neema, na si kwa
matendo ,
lakini tunda lake ni utii wa amri kumi . Hutii
huu hukuza tabia ya kikristo na huwa na
matokeo ya ustawi . Ni ushuhuda wa upendo
wetu kwa Bwana na wajibu kwa ajili ya
wanadamu wenzetu . Utii wa imani
udhihirisha uwezo wa kristokubadilisha
maisha, na
hivyo huimarisha ushuhuda wa kristo. ( Kut
20 : 1 - 17 , Zab40 : 7, 8 Math 22 : 36 -40 Kumb28 : 1 -
14 Math 5 : 17 -20 , War 8 : 3 ,4 Zab 19 : 7 - 14 )
20 . Sabato
Muumbaji mkarimu, baada ya siku sita za
uumbaji, alipumzika siku ya saba na
kuanzisha
sabato kwa ajili ya watu wote kama
kumbukumbu ya uumbaji . Amri ya nne ya
sheria za
Mungu zisizobadilika inaagiza adhimisho la
sabato hii ya siku ya saba kama siku ya
mapumziko , ibada , na huduma kulingana na
mafundisho na uzoefu wa Yesu , Bwana wa
sabato. Sabato ni siku ya mawasiliano yenye
furaha pamoja na Mungu na sisi kwa sisi . Ni
mfano wa ukombozi wetu katika kristo ,
ishara ya utakaso wetu , ishara ya utii wetu ,
na
mwonjo wa umilele wetu wa siku zijazo
katika ufalme wa Mungu. Sabato na ishara ya
daima
ya mungu ya agano la milele la Mungu kati
yake na watu wake. Utunzaji wa furaha wa
wakati huu mtakatifu toka jioni hadi jioni, jua
kuchwa hadi jua kuchwa, ni adhimishola
matendoya Mungu ya uumbaji na ukombozi .
( Mwa 2 : 1 - 3, Kut20 : 8- 11 , Luka 4 : 16 , Isay56 : 5 -
6, 58 : 13 - 14 , Math 12 : 1- 12 , Ezek20 : 12 -20 ,
Kumb5 : 12 -15 , Wal23 : 32 , Marko 1 : 32 ) .
21 . Uwakili
Sisi tu mawakili wa Mungu, tuliokabidhiwa
nay eye wakati na fursa , uwezo na mali , na
mibaraka ya dunia na raslikamali zake .
Tunawajibika kwake kwa matumizi yake
sahihi.
Tunakiri umilikaji wa Mungu kwa huduma ya
uaminifu kwake na kwa wanadamu wenzetu ,
na kwa kurudisha Dhaka na kutoa sadaka
kwa ajili ya utangazaji wa injili yake na kwa
utegemezaji na ukuaji wa kanisa lake .
Uwakili ni fursa iliyotolewa kwetu na Mungu
kwa ajili
ya malezi katika upendo na ushindi dhidi yao
choyo na tama . Wakili kufurahia mibaraka
inayowajia wengine kama matokeo ya
uaminifu wake. ( Mwa 1 : 26 -28 , 2 : 15 ,
1Nyak 29 : 14 ,
Hagai 1 : 3 - 11 , Malak 3 : 8 -12 , 1Wakor 9: 9- 14 ,
Math 23 : 23 , 2Wakor 8 : 1 -15 Warumi 15 : 26 - 27 . ) .
22 . Mwenendo wa kikristo
Tumeitwa kuwa watauwa wanaofikiri ,
kujisikia , na kutenda kutenda kulingana na
kanuni za
mbinguni. Ili Roho aumba ndani upya ndini
yetu tabia ya Bwana wetu tunajihusisha tu
katika mambo yale ambayo yatazaa katika
maisha yetu usafi unaofanana na kristo , afya ,
na
furaha katika maisha yetu . Hii inamaanisha
kwamba maraha na maburudisho yetu
yanapaswa kufikia viwango vikuu vya maonji
na uzuri wa kikristo . Huku tukitambua
tofauti
za kitamaduni , mavazi yetu yanapaswa yawe
ya kawaida , si ya anasa , na safi, yanayostahili
wale ambao uzuri wao wa asili yake si
mapambo ya nje, bali asili yake ni mapambo
yasiyoharibika , yenye roho ya upole na
utulivu . Pia inamaanisha kwamba kwa kuwa
miili
yetu ni maekalu ya Roho mtakatifu,
tunapaswa kuitunza kwa akili . Pamoja na
mazoezi
tosha na mapumziko , yatupasa kuchagua lishe
yenye afya sana kadiri inavyowezekana na
kuepuka vyakula visivyo najisi , vilivyotajwa
katika maandiko matakatifu . Kwa vile
vinywaji
vya vileo , tumbaku na matumizi mabaya ya
madawa hudhuru miili yetu, yatupasa
kuepukana nayo pia. Badala yake yatupasa
kujishughulisha na chochote kile
kitakacholeta
mawazo yetu na miili yetu yawe katika
nidhamu ya kistro, ambaye hutamani uzima
wetu ,
furaha , na wema . ( Warumi 12 : 1 -2 , 1 Yoh 2: 6,
Waef 5: 1; 21 , Wafil 4 : 8 , 2 Wakor 10 : 5, 6 : 14 ,
7: 1, 1 Pet 3: 1- 4 , Walawi 11 : 1 -47 , 3 Yoh . 2)
23 . Ndoa na Familia
Ndoa ilianzishwa Edeni na Mungu na
ikasibitishwa na Yesu kuwa muungano wa
maisha
yote kati ya mwanaume na mwanamke katika
wenzi wenye upendo . Kwa mkristo kifungo
cha ndoa ni kwa Mungu na pia kwa mwenzi ,
na kishirikiwe tu na wenzi wenye imani
moja .
Upendo wa hiari, heshma , staha , na
uwajibikaji ndizo fito za { kujenga } uhusiano
huu,
ambao utaakisi upendo , utakatifu , ukaribu ,
uthabiti wa uhusiano kati ya kristo na kanisa
lake. Kuhusu talaka , Yesu alifundisha
kwamba mtu anayemwacha mwenza ,
isipokuwa kwa
sababu ya uasherati, na akaoa { au kuolewa }
na mwingine azini . Ingawa baadhi ya
mahusiano ya kifamilia huenda yakashindwa
kufikia lengo , wenzi katika ndoa ambazo
wamejitoa kikamilifu kila mmoja kwa
mwenzake katika kristo wanaweza kufaulu
kufikilia
katika umoja wenye upendo kupitia uongozi
wa Roho na malezi ya kanisa . Mungu
hubariki
familia na anakusaidia kwamba washirika
wake watasaidiana wao kwa wao kufikia
upevu
kamili . Wazazi wawalee watoto wao katika
kumpendeza na kumtii Bwana . Kwa kielelezo
chao na maneno yao wawafundishe kwamba
kristo ni mtiishaji mwenye upendo , daima
mpole na mwenye kujali, anayetaka wawe
kiungo katika mwili wake, familia ya Mungu.
Kukuza ukaribu wa mahusiano wa kifamilia
ni moja wapo ya alama{ ya kujulisha } ujumbe
wa
mwisho wa injil. ( Mwa 2 : 18 -25 , Math 19 : 3- 9,
Yoh 2 : 1 -11 , 2Wakor 6 : 14 , Waef 5 : 21 -33 , Luka
16 : 18 , 1Wakor 7 : 10 -11 , Kut20 : 12 , Kumb6 : 5- 9,
Mith22 : 6 , Mal 4 : 5 -6 )
24 . Huduma ya Kristo katika Hekalu la
Mbinguni
Kuna hekalu mbinguni , hema la kweli
lililosimamishwa na Bwana na siyo
mwanadamu .
Ndani yake kristo anahudumu kwa niaba
yetu, akiwezesha kupatikana kwa ajili ya
waumini
fanaka za kafara yake ya upatanisho
iliyotolewa mara moja msalabani kwa ajili ya
wote .
Alizinduliwa kuwa kuhani wetu mkuu na
akaanza huduma yake ya uombezi wakati wa
kupaa kwake mbinguni. Mnamo mwaka 1884 ,
mwishoni mwa kipindi cha unabii wa siku
2300, aliingia katika awamu ya pili nay a
mwisho katika huduma yake ya upatanisho .
Ni
kazi ya hukumu ya upelelezi ambaya ni
sehemu ya mwisho ambayo hatimaye
itakomesha
dhambi yote , iliyokuwa mfano wa kutakaswa
kwa hekalu la kale la waebrania katika siku
ya
upatanisho . Katika huduma hiyo kielelezo
hekalu lilitakaswa kwa damu ya wanyama wa
kafara , likini mambo ya mbinguni hutakaswa
kwa kafara kamilifu ya damu ya Yesu .
Hukumu ya upelelezi kufunua kwa viumbe
wa mbinguni ni nani miongoni mwa wafu
wamelala katika kristo na hivyo , katika yeye
wanahesabiwa kustahili kuwa na sehemu
katika
ufunuo wa kwanza . Pia inadhihirisha zazi ni
nani miongoni mwa walio hai wanakaa ndani
ya kristo , wakishika amri za Mungu na imani
ya Yesu , na katika yeye, hivyo basi, wako
tayari kwa ajili ya kuhamasishwa kuingia
katika ufalme wa milele . Hukumu hii
huthibitisha
haki ya Mungu, katika kuwokoa wale
wanaomwamini Yesu . Hutangaza kwamba
wale
waliohudumu kuwa watiifu kwa Mungu
watapokea ufalme . Hitimisho ya huduma hii
ya
kristo itakuwa ndiyo mwisho wa kufunga
mlango wa rehema ya mwanadamu kabla ya
marejeo ya Yesu . ( Waebr 8 : 1 -5 , 4 : 14 -16 ,
9: 11 - 28 , 10 : 19 -22 , 1 : 3 , 2 : 16 - 17 . Dan 7: 9- 27 ,
8: 13 -
14 , 9: 24 - 27 . Hes 14 : 34 . Ezekl 4 : 6 Ufu 14 : 6 -7 ,
20 : 12 , 14 : 12 , 22 : 12 . )
25 . Kuja kwa Kristo mara ya pili
Kuja kwa kristo mara ya pili ndilo tumaini
lenye baraka la kanisa , hitimisho kuu la injili.
Kuja kwa mwokozi kutakuwa halisi, binafsi ,
kutaonekana kwa dunia mzima . Atakaporudi
wenye haki waliokufa watafufuliwa na
pamoja na wenye haki walio hai watavikwa
utukufu
na kuchukuliwa kwenda mbinguni , lakini
waovu watakufa . Kutimizwa karibu kabisa
kwa
sehemu nyingi za unabii , pamoja na hakli ya
sasa ya ulimwengu , huonyeshe kwamba kuja
kwa kristo ku karibu sana . Wakati wa tukio
hilo hakukufunuliwa , na hivyo basi
tunahimizwa kuwa tayari kwa nyakati zote . .
( Tito 2: 13 , Math 24 , Mdo 1 : 9 -11 , Math 24 : 14 ,
Ufu 1: 7 , 14 : 14 - 20 , Math 24 : 43 - 43 ,
Wakor 15 : 51 -50 , 1 Wathes 1 : 7 , 4: 13 - 18 , 5: 1 -6 ,
Marko 13 ,
Luka 21 : 2, Tim 3: 1 -5 ) .
26 . Mauti na Ufunuo
Mshahara wa dhambi ni mauti . Lakini
Mungu, ambaye peke yakehapatwi na mauti ,
atawapa uzima wa milelewaliokombolewa
wake. Mpaka siku hiyo mauti ni hali ya
kutokuwa na fahamukwa watu wote . Wakati
kristo, aliye uzima wetu , atakapotokea , wenye
haki waliofufuliwa na walio hai watafikwa
utukufu na kunyakuliwa juu ili kumlaki
Bwana
wao . Ufufuo wa pili ambao ni ufufuo wa
waovu, utatokea miaka elfu moja baadaye .
( Warum 6 : 23 , 1Tim 6 : 15 -16 , Mhu 9 : 5 -6 , Zab
149: 3 -4 , Yoh 11 : 11 - 14 , 1 Wakor 15 : 51 -54 ,
1Wathes 4 : 13 -17 , Ufu 20 : 1 -10 )
.
27 . Milenia { Miaka Elfu} na Mwisho wa
Dhambi
Milenia ni miaka elfu moja ya utawala wa
kristo pamoja na watakatifu wake mbinguni
kati
ya ufufuo wa kwanza na pili . Wakati huo
waovu waliokufa watahukumiwa , dunia
itakuwa
ukiwa na utupu , bila wanadamu wakazi walio
hai , lakini ikikaliwa na shetani na malaika
zake . Mwishowe kristo na watakatifu wake na
Mji Mtakatifu watashuka kutoka Mbinguni.
Ndipo waovu waliokufa watafufuliwa, nao
pamoja na shetani na malika zake
watauzingira
mji , Lakini moto kutoka mbinguni
utawateketeza ili kuitakasa dunia. Na hivyo
ulimwengu
utakuwa huru bila dhambi na wenye dhambi
milele. ( Ufu 20 , 1 Wakor 6 : 2 -3 , Yer 4 : 23 -26 ,
Ufu 21 : 1 -5 ,Mal 4: 1, Ezekl 28 : 18 -19 )
28 . Dunia Mpya
Katika dunia mpya , ambamo haki
hukaa, Mungu ataweka tayari makao ya milele
waliokombolewa na mazingira makamilifu
kwa maisha ya milele, upendo , furaha na
kujifunza mbele zake . Kwa hapa Mungu
mwenyewe atakaa pamoja na watu wake, na
taabu
na mauti vitakuwa vimepita . Pambano kuu
litakuwa limemalizika, na dhambi
haitakuwepo
tena. Vitu vyote vyenye uhai na visivyo na
uhai vitatangaza kwamba Mungu ni pendo,
naye
atatawala milele. Amina . ( 2 Pet 3 : 13 , Isa 35 ,
65 : 17 -25 , Math 5: 5 , Ufu 21 : 1 -7 , 22 : 1 -5 , 11 : 5) .
Ijumaa, 27 Mei 2016
Kanuni za Kanisa la Sda
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni