Alhamisi, 30 Juni 2016

Mwenyekiti SHC apata ajari.

Breaking news.  Mwenyekiti wa Conference ya Nyanda za Juu Kusini (STUM) Mchungaji Kenan Mwasomola Amepata Ajali Mida ya Saa 2 Usiku wajana Tarehe 29/06/2016 eneo la Nyandekwa Katikati ya Igunga na Nzega Wakati Akielekea Kirumba Mwanza kwa Sherehe ya Jubilee ya miaka 50 akiwa na Gari la Office.

Kwa Mujibu wa Taarifa ya Shuhuda wa Ajali hii Ambaye pia alikuwa ndani ya Gari hilo Mch. D Bambaganya Amesema Mwenyekiti Ameumia Maeneo ya Mbavu na Mke wa Mwenyekiti Ameumia Shingoni na Begani na Tayari wote wamelazwa  Hospitali ya Mission ya Nkinga Na hali zao Zinaendelea Vizuri.

Sababu ya Ajali inasemekana ni Tuta lililo kuwa katika barabara ambayo lami imekwanguliwa na Kulikuwa hakuna alama yeyote ya kuelekeza. Jambo lililo sababisha Gari kubilingita juu chini na hatimaye kusimama.

Kwa Mujibu wa wenyeji wa eneo hilo wanasema Tuta hilo limesha sababisha Ajali nyingi zilizo poteza maisha ya watu. Tena hata asubuhi hii wakati nikipokea Habari hizi kunagari jingine dogo limeponapona kupata Ajali mbaya.

Tuendelee Kumuombea Mwenyekiti na Majerui wote ili BWANA awaponye na kuendelea na Kazi katika kipindi hiki cha Utume kwanza ni wakati wa mavuno. Amen

By. Mchungaji Haruni Kikiwa - Mbalizi District Pastor SHC

Lessoni Alhamis, Jukumu la kanisa la urejeshaji.

🌳LESSON 🌳

🌲Alhamisi june 30 🌲

Jukumu la kanisa la urejeshaji.


🌲kama tulivyoona, Ulimwengu wetu, ingawa uliumbwa mkamilifu, ulianguka, kwa matokeo yenye kuleta uharibifu mkuu. Lakini mungu hakutuacha katika kile ambacho kingelikuwa hatima yetu, kuangamia milele,(hatima ambayo sayansi inasema inatungojea). Badala yake, hata kabla Ulimwengu haujakuwapo, mpango wa wokovu uliundwa, (angalia 1 pet, 1 :2) na kwa gharama kubwa isiyopimika kwake (Mungu), Yesu alikuja katika Ulimwengu huu na kuteseka msalabani na aliahidi kuwa atarudi. Wakati ambapo kila kitu kitakuwa kimepita na dhambi imeangamizwa, Ulimwengu ule uliokuwa umepotea utarejeshwa upya kikamilifu.

🌲Hata hivyo, kinachoshangaza ni kwamba hata sasa mungu anatuita sisi, kanisa lake, kuwa na sehemu ya kazi ya kufanya katika kuelekea kwenye urejeshwaji huu.

   Soma marko 2:1-12 kisa cha jinsi ambavyo marafiki fulani kwa uthabiti walifanya kazi  kwa   pamoja katika kumpeleka aliyekuwa amepooza kwa Yesu. Ni kwa jinsi gani kisa hiki kinaelezea wajibu wa kanisa katika uponyaji na urejeshaji upya wa watu?



🌲Nyumba ilikuwa imejaa watu kwa sababu Yesu Alikuwa pale. Upendo wake kwa watu uliwavuta makutano. Wale watu wanne waliotoboa tundu kwenye paa ili kumfikisha kwa Yesu huyu mtu aliyekuwa mgonjwa wa kiroho, kiakili, na kimwili. Ndipo Yesu alipomrejesha upya mtu huyo kwa kusamehe dhambi zake, kumpatia amani moyoni na kumwamuru kusimama na kutembea. Yesu alidhihirisha kwamba hakuna mtu anakuwa ameponywa kwa hakika isipokuwa amerejeshwa upya katika kila jambo.

  Mtume Yohana  alielezeaje sababu ya Kristo kuja humu duniani? Tunaweza kupata tumaini gani kutoka kwenye ahadi hizi? Soma yohana. 10:10, 1 yoh. 3:8.



🌲Imeelezwa kuwa yohana 10:10 ni muhtasari wa ujumbe wa waadventista wa sabato. Kwa uwazi hili ndilo lililokuwa tamko la utume la Yesu. Jukumu kuu la mwili wa kristo, kanisa lake, halina budi kufuata nyayo zake na kuziharibu kazi za yule mwovu kwa kubadilisha mauti na mahali pake  kujazwa kwa uzima tele,  (angalia Mdo. 10:38:,1 yoh. 2:6).kanisa limeitwa kufanya kazi kwa ubia na kristo kwa kuwasukuma watu kuelekea kwenye  kurejeshwa upya katika sura ya Mungu-kimwili, kiakili na kiroho.

👫Ni watu gani ambao kwa sasa wanahitaji msaada wako, Msaada ambao kwa namna ya pekee umeandaliwa ili uweze kutoa?

Jumatano, 29 Juni 2016

Lessoni j5 UREJESHWAJI KATIKA KRISTO.

🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻
☂☂☂☂☂☂☂☂☂☂☂
   Lesson ya leo Jumatano,  Jun 29.

Somo!!  UREJESHWAJI KATIKA KRISTO.

'' 👉🏾 Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpka Kristo aumbike ndani yenu'' (Gal. 4:19).👈🏽

--------------------------------
✍🏽⏩ Kwa asili, tuliumbwa tukiwa viumve wakamilifu na watimilifu kwenye Ulimwengu mkamilifu na mtimilifu. Kwa bahati mbaya, paradiso hii ya kabla ya Anguko ilipotezwa kwa njia ya dhambi, na ulimwengu huu tunavyoufahamu kwa sasa,  Umejaa vifo, vurugu, mateso, hofu, na ujinga. Mpango wa wokovu uliasisiwa ili kuurudisha ulimwengu huu katika ukamilifu wake wa Asili.
Kristo alikuja ili kukirejesha kilichokuwa kimepotezwa wakati wa Anguko.

✍🏽⏩ '' Hapo mwanzo Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake mwenyewe.
Alimjalia kwa sifa au tabia zilizo bora. Akili yake ilikuwa katika ulinganifu mkubwa, na uwezo wake wote uliokuwa ndani yake  ulikuwa katika upatanifu.  Lakini Anguko na madhara yake vimepotosha  vipawa hivi.

✍🏽 Dhambi imeharibu na ilikuwa karibu kabsa kuifuta sura ya Mungu kutoka kwa mwanadamu. Ilikuwa ni katika kuirejeaha upya  ndipo mpango wa wokovu ulibuniwa,,  na mwanadamu alipewa maisha ya majaribio. Kumrejesha upya katika ukamilifu aliokuwa ame7mbwa nao hapo mwanzo na hili ndilo kusudi kubwa la maisha - kusudi lililo la msingi kwa mengine yote.'' E.G White, patriarchs  and prophets, Uk 595.
Ingawa urejeshwaji upya huu hautakamilika  mpaka wakati wa mbingu mpya na nchi mpya, mchakato huo umekwisha  kuanza ndani yetu sasa!!.

Soma👉🏾 Wagalatia 4:19. Chochote kile alichokuwa anataka kujihusisha  nacho wakati huo, ni wazo gani muhimu la Kiroho Paulo analilenga hapa?
--------------------------------
✍🏽 Katika vitabu vya Waebrania 1:3 Yesu anatambulishwa kama sura ya Mungu, '' Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe '' (BHN)

(Linganisha na Yn 14:9; 2Kor:4:4; Kol.1:15). Anatamani kulingana nasi ili kuirejesha upya sura ya Mungu ndani yetu. Ikiwa tutakubali, Kristo aliye Sura ya Mungu atakuwa ndani yetu; ''Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo linamaanisha kwamba, ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu. (Kol. 1:27 BHN).

✍🏽⏩ Uzoefu wa mwisho wa kurejeshwa upya katika sura yake utatokea wakati wa ujio wa pili wa Yesu.  (Soma 👉🏾1kor. 15:49, 1Yoh. 3:2). Hata hivyo, Kristo anapokuwa ndani yetu, nasi ndani yake, mchakato wa Kurejeshwa upya katika Sura ya Mungu unaanza tukiwa upande huu wa kurejeshwa upya katika sura ya Mungu unaanza tukiwa upande huu wa mbingu. Na jambo hilo linapotokea, tutakuwa na shauku ya kuwaleta wale walio katika jamii zetu kwake yeye anayeweza kuwarejesha upya na wao pia.

(MATUMIZI MAISHANI )

👉🏾 Ingawa kazi hiyo, ya kuturejesha upya, inaanza ndani yetu sasa, kwa nini siku zote inatupasa kukumbuka kuwa urejeshwaji upya hautakamilika hadi ujio wa pili wa Yesu?
            '' MWISHO''

🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻🌻
☂☂☂☂☂☂☂☂☂☂☂

Jumatatu, 27 Juni 2016

Lessoni J3. Anguko na Matokeo yake.

Jumatatu :usomaji wa Biblia :1Nyakati 14    juni 27

🙊ANGUKO NA MATOKEO YAKE 🙈

✍🏾Biblia haisemi kuwa ulipita muda gani toka Uumbaji ulipokamilika na Anguko. Hatujui ni muda gani ulipita, siku, majuma, au miaka.
✍🏾 Hata hivyo, kile tunachofahamu ni kwamba, kulikuwa na Anguko, na matokeo yake yalikuwa ya mara moja na yalikuwa dhahiri.
✍🏾Matokeo yaliotajwa mwanzoni ya Adamu na Hawa kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya yalikuwa ni utambuzi wao wa ghafla kuwa walikuwa uchi (Mwa. 3:7). Walitafuta kujificha kutoka mbele za Mungu. Mavazi yao ya nuru sasa yakiwa yametoweka. (angalia patriarchs and prophets cha Ellen G. White uk. 57). Uhusiano wao wa karibu waliokuwa nao kwa Mungu wao ulivurugwa kwa sababu ya uhusiano wa karibu mpya waliougundua kwa ubinafsi wa uovu. Kwa hiyo Mungu akatafuta kuwaelimisha wanandoa hawa wa kwanza kuhusiana na matokeo yaliosababishwa kwao na Dhambi yao.

SOMA aya zifuatazo na utambue matokeo ya mara moja ya dhambi ya Adamu na Hawa kama inavyoonekana katika kila fungu la maneno.
Vile vile ni kwa namna gani matokeo yake Yale yanadhihirika leo?

Mwa. 3:8-10......................

Mwa. 3:12..............................

Mwa. 3:13.................................

Mwa. 3:16................................

Mwa. 3:17-19..........................

----------------------—
✍🏾Hakuna shaka, Anguko lilikuwa halisi, Anguko lilikuwa kitu kibaya, Anguko lilikuwa na matokeo mabaya na ya kusikitisha kwa jamaa ya wanadamu. Kisa kirefu na cha kusikitisha cha historia ya mwanadamu tangu wakati huo hadi kwenye matukio ya wakati huu, yanafunua matokeo mabaya na ya kusikitisha ya dhambi.

✍🏾Inatupasa kuwa na shukrani kiasi gani kwa ahadi kuwa siku moja msiba wa dhambi utamalizika na kutokomezwa usijirudie kamwe.

🌑Ni kwa namna gani tunaishi kila siku kwenye matokeo ya dhambi zetu?

✅✅✅✅✅✅✅✅✅✅✅

Lessoni J3. Anguko na Matokeo yake.

Jumatatu :usomaji wa Biblia :1Nyakati 14    juni 27

🙊ANGUKO NA MATOKEO YAKE 🙈

✍🏾Biblia haisemi kuwa ulipita muda gani toka Uumbaji ulipokamilika na Anguko. Hatujui ni muda gani ulipita, siku, majuma, au miaka.
✍🏾 Hata hivyo, kile tunachofahamu ni kwamba, kulikuwa na Anguko, na matokeo yake yalikuwa ya mara moja na yalikuwa dhahiri.
✍🏾Matokeo yaliotajwa mwanzoni ya Adamu na Hawa kula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya yalikuwa ni utambuzi wao wa ghafla kuwa walikuwa uchi (Mwa. 3:7). Walitafuta kujificha kutoka mbele za Mungu. Mavazi yao ya nuru sasa yakiwa yametoweka. (angalia patriarchs and prophets cha Ellen G. White uk. 57). Uhusiano wao wa karibu waliokuwa nao kwa Mungu wao ulivurugwa kwa sababu ya uhusiano wa karibu mpya waliougundua kwa ubinafsi wa uovu. Kwa hiyo Mungu akatafuta kuwaelimisha wanandoa hawa wa kwanza kuhusiana na matokeo yaliosababishwa kwao na Dhambi yao.

SOMA aya zifuatazo na utambue matokeo ya mara moja ya dhambi ya Adamu na Hawa kama inavyoonekana katika kila fungu la maneno.
Vile vile ni kwa namna gani matokeo yake Yale yanadhihirika leo?

Mwa. 3:8-10......................

Mwa. 3:12..............................

Mwa. 3:13.................................

Mwa. 3:16................................

Mwa. 3:17-19..........................

----------------------—
✍🏾Hakuna shaka, Anguko lilikuwa halisi, Anguko lilikuwa kitu kibaya, Anguko lilikuwa na matokeo mabaya na ya kusikitisha kwa jamaa ya wanadamu. Kisa kirefu na cha kusikitisha cha historia ya mwanadamu tangu wakati huo hadi kwenye matukio ya wakati huu, yanafunua matokeo mabaya na ya kusikitisha ya dhambi.

✍🏾Inatupasa kuwa na shukrani kiasi gani kwa ahadi kuwa siku moja msiba wa dhambi utamalizika na kutokomezwa usijirudie kamwe.

🌑Ni kwa namna gani tunaishi kila siku kwenye matokeo ya dhambi zetu?

✅✅✅✅✅✅✅✅✅✅✅

Jumapili, 26 Juni 2016

TIPS ON HOW TO REMAIN POOR* (Prof. Makau)

*
*1. _Never wake up early._* Keep stretching and turning in bed until you get too hungry to continue dozing. If there are no bed bugs, why hurry to get up?

*2. _Never plan how to spend your money._* Whenever you get money, start spending it right away and when it's finished, you try to count and recall how you spent it.

*3. _Don't think of saving until you have real big money._* How can you save when you earn so little? Those telling you to save are not sympathetic to your burning needs.

*4. _Don't engage in activities usually reserved for the "uneducated"._* How can you, a graduate, engage in petty trade, network marketing or home-based production? That's for people who never went to school!

*5. _Don't think of starting a business until an angel comes from heaven and gives you capital._* How do they expect you to invest before you get millions? Even though more than half the businesses in your town were started with little capital, you as a smart person can only start with millions.

*6. _Complain about everything except your own attitude and laziness._* Blame the system, the government and the banks that refused to lend you money. They are all bad and do not want you to get rich.

*7. _Spend more than you earn._* To achieve this, buy consumer products on credit and keep borrowing from friends and employers.

*8. _Compete in dressing._* Make sure you're wearing the latest clothes. Intimidate the congregation with your trendy fashions every Sunday. Whenever your neighbour buys a new phone, you get one that is more expensive.

*9. _Get yourself a nice second hand car_* that costs more than three times your yearly salary.

*10. _Give your children everything they ask for since you're such a loving parent._* They should not struggle for anything because you do not want them to suffer that way, they will grow up lazy and hence poor enough to ensure they can't help you at old age

Lessoni jumapili

*JUMAPILI  JUNE 36 2016*

*MFANO WA MUNGU*

Biblia inasema kuwa, kwa asili, mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu. (Mwanzo 1:27). Umbo linaweza kuwa la kutazamwa kwa pande mbili, kama vile kuakisi kwa kioo au nakala ya picha, au kutazamwa kwa pande tatu, kama vile sanamu au picha ya pande tatu inaytokana na maingiliano ya mionzi ya nuru. Wakati mwingine sura au mfano huwa ni kitu kisicho halisi, kama vile picha ya mawazoni, dhana tunayokuwa nayo akilini. Biblia inamaanisha nini?

*Soma Mwanzo 1:26, 27. Maandiko yanafafanuaje juu ya kuumbwa kwa sura ya Mungu? Angalia pia Mwanzo 1:31, Kumb. 6:5, na 1Thes. 5:23.*

Kwa kuumbwa kwa wazazi wetu wa kwanza, Mungu aliweka kiwango kipya kwa ajili ya maisha duniani: mwanamume na mwanamke. Wao peke yao, miongoni mwa viumbe vingine vyote vilivyoumbwa wakati huo, walikuwa na mfano wa Mungu. Hawakuwa manyani waliobadilika na kuwa binadamu. Kama Wanadamu, wao pamoja na sisi kimsingi tuko tofauti kabisa na aina zingine zote za viumbe duniani, na teolojia yoyote inayohafifisha tofauti hii inamdhalilisha mwanadamu.

"Mungu akawaita jina lao Adamu" (Mwanzo 5:2). Yaani, wote wawili mwanamume na mwanamke, ijapo wako tofauti kabisa kila mmoja kwa mwenzake, hata hivyo bado walikuwa ni mmoja. Kwa pamoja, katika ukamilifu na utimilifu wao, walikuwa wakiiwakilisha sura ya Mungu.

Asili ya sura ya Mungu ni jumuishi: "Adamu alipotoka katika mikono ya Mwumbaji, alikuwa amebeba, katika asili yake ya kimwili, kiakili, na kiroho, mfano wa Muumba wake." - Ellen G. White, Education uk. 15.

Neno linalosimama "sura" katika Kiebrania ni tselem; na neno linalosimamia "mfano" ni demuth. Maneno hayo yanaweza kumaanisha umbile la kimwili na kiakili vya mwanadamu. Ellen G. White analitambua hilo anaposema mwanadamu aliumbwa katika sura ya Mungu "ni katika kufanana kwa sura ya nje na katika tabia pia." - Patriachs and Prophets, uk. 45.

Kumbukumbu la Torati 6:5 huzitaja nyanja mbalimbali zilizomo ndani ya mwanadamu: roho (mambo ya kiroho), moyo (akili, utambuzi), na nguvu; (yaani mwili). Kuna mpangilio kama huo pia katika 1Thes. 5:23. Mwanadamu aliyeumbwa kwa sura ya Mungu kwa asili angejumuisha vitu vyote hivyo vyote ndani yake.

*"Ijapokuwa Kuna mengi zaidi juu ya dhana hii ya kuumbwa katika "sura ya Mungu," Biblia iko wazi kuwa: binadamu ni kiumbe tofauti na wa pekee katika viumbe vyote hapa duniani. Hakuna kiumbe kingine chochote kilicho karibu naye. Kwa nini ni muhimu kwetu kuidumisha tofauti hiyo akilini?*

Lessoni sabato mchana.

🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳🌳
      Juni 25-Julai 1

''UREJESHWAJI UPYA WA VITU VYOTE''

Sabato Mchana.
Somo la Juma Hili: Mwa. 1:26,27; Kum.6:5; Mwa. 3:8-19; Yak.4:4; Gal.4:19; Marko 2:1-12; Yoh. 10:10.

FUNGU LA KUKARIRI: 
'' Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.'' (Mwanzo 1:27).

⏩✍🏽  Kile kinachompasa Mtu kufanya ni kutazama kila upande unaomzunguka,
Kuuangalia Ulimwengu, katika ujirani, kujitazama yeye mwenyewe ili kuliona jambo hili.

⏩ Na jambo hili ni lipi? Jambo fulani limekwenda vibaya sana.
Jambo hili linaitwa Anguko,  linaitwa dhambi,  linaitwa Uasi, na linaitwa Pambano Kuu.

⏩✍🏽 Hata hivyo, Habari njema ni kwamba, Jambo hili si la kudumu. Halitakuwepo siku zote. Yesu alikuja na kufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu na aliahidi kuja tena,
⏩ na atakapokuja tena,,, hakuna hakuna jambo lolote la dunia hii litakalosalia. Badala yake, Ufalme mpya, Ufalme wake wa milele utaanza. '' Na katika siku za Wafalme hao Mungu wa Mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele'"" (Dan 5:44).
Urejeshwaji upya wa kushangaza kiasi gani!!

⏩✍🏽 Lakini hatutangoja hadi Ujio wa pili kwa ajili ya Urejeshwaji Upya kuanza. Wale walio katika Kristo ni viumbe vipya kwa sasa. (2Kor 5:17). na tumechaguliwa ili tufuatishe na kufananishwa na mfano wa Yesu sasa.
(Rum 8:29). Pia, yeye anatuita na kutuwezesha, kama kanisa lake ili kwamba tuweze kufanya kazi ambayo itawarejesha watu wengine pi.

          Mwisho.
Karibuni kwa michango na maswali kwa Lesson ya leo,  Kuchangia kwenu ndo kupanuka kwa Maarifa ya Kimbingu.

📖📖📖📖📖📖📖📖📖
🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾🙏🏾

Jumamosi, 25 Juni 2016

Somo la 13: Msulubiwa na Mfufuka

Utangulizi:
Somo letu la Mathayo juma hili
linawamulika wasaliti wawili na mwanamke
mmoja aliyejitoa kikamilifu kwa Yesu. Je,
inamaanisha nini hasa kumsaliti Yesu?
Inamaanisha nini kujitoa kikamilifu kwa
Yesu? Kwa nini matokeo ni tofauti sana kwa
msaliti mmoja kuliko mwingine? Hebu
tuzame kwenye somo letu la Biblia ili
tujifunze zaidi!
I. Wapanga Njama na
Mwanamke
A. Soma Mathayo 26:1-2. Kwa
dhahiri hizi ni habari zenye kukatisha
tamaa sana. Kwa nini uwaambie wanafunzi?
(Yesu alitaka kuwaonya (kwa mara nyingine
tena).)
1. Hiyo inaashiria nini kuhusu
umuhimu wa matukio ya siku za mwisho?
(Yesu atatuonya kuhusu matukio ya
muhimu na yale yenye changamoto.)
B. Soma Mathayo 26:3-7. Tunazo
taswira mbili kinzani. Taswira ya kwanza ni
ya kundi linalopanga kumwua Yesu na
nyingine ni ya mwanamke ambaye anajitoa
kwa hali ya juu kwa ajili ya Yesu. Kutokana
na Yesu kuelewa mustakabali wa mauti
yanayomkabili kitambo kifupi kijacho,
unadhani alijisikiaje kuhusu huyu
mwanamke? (Hii ni nyota inayong’aa
kwenye mazingira ya giza. Ningemshukuru
sana mwanamke huyu.)
C. Soma Mathayo 26:8-9.
Unauelezeaje mwitiko wa wanafunzi?
Wameambiwa kwamba Yesu anakaribia
kufa, je, hawapaswi kushiriki katika
kumfanyia jambo la pekee? (Nadhani
wanafunzi walipingana na uhalisia kwa
kutokubali kuamini kile alichowaambia
Yesu. Hawakutaka kuamini kuwa atakufa.)
1. Je, ungekuwa na mwitiko gani
endapo wewe ndiye ungekuwa huyu
mwanamke na kusikia ukosoaji huu?
Umejitoa kwa kununua hii marhamu, na
sasa wanafunzi wanakukosoa!
2. Kuna dhana katika fungu hili
ambayo nataka uiangalie. Wanafunzi
hawakusema kwamba mwanamke alipaswa
kutoa fedha kwa masikini badala ya
kununua marhamu, bali walisema kuwa
angeweza kuiuza hiyo marhamu. Hii
inatuambia nini kuhusu jinsi mwanamke
huyu alivyoipata hii marhamu? (Ilikuwa ni
zawadi. Kwa uthibitisho, hakikuwa kitu
ambacho angeweza kumudu kukinunua.)
D. Soma Mathayo 26:10-13. Hii
ilikuwa ni zawadi, kuna mtu alidhamiria
mwanamke huyu aweze kuitumia zawadi
hiyo. Badala yake, alichagua kujikana nafsi
kwa kutoitumia kama walivyopendekeza
wanafunzi. Je, wanafunzi walikuwa na haki
ya kumwambia kufanya matumizi
anayopaswa kujikana nafsi ili kutoyafanya?
(Hawana ushauri sahihi. Yesu anasema
kuwa alichokifanya mwanamke huyu
kitaongelewa katika kumbukumbu lake na
historia yote.)
1. Je, zipo fursa
zinazokuzunguka kuinua mioyo ya watu
waliokata tamaa kwa kuwatendea wema?
2. Je, pia watazungumzia
duniani kote kuhusu habari ya wanafunzi
kumkosoa mwanamke huyu aliyejikana
nafsi?
3. Kuna tofauti gani kati ya
mtazamo wa mwanamke na ule wa
wanafunzi? (Alikuwa amejitoa kwa Yesu
kikamilifu. Wanafunzi walijitoa kufanya
uamuzi wa matumizi bora ya marhamu
yake.)
II. Yuda
A. Soma Mathayo 26:14-16. Je,
Yuda ndiye aliyemkosoa mwanamke?
1. Unadhani kwa nini Yuda
alimsaliti Yesu? Je, sasa aliamua kumchukia
Yesu? (Ninazo nadharia mbili. Kwanza,
hakuamini kwamba Yesu angeweza kuuawa
– na kwamba angeweza pia kupokea fedha
kama thawabu kwa kumlazimisha Yesu
kujitangaza kuwa Mfalme. Pili, kwamba
Yesu alimaanisha sana juu ya kifo chake,
kiasi kwamba alistahili fedha kwa muda
alioupoteza kwa kuzunguka kwake kote kwa
muda wa miaka mitatu. Katika nadharia
zote mbili, alijitumainia yeye mwenyewe na
wala hakumtumaini Yesu.)
2. Soma Mathayo 18:7. Je,
maelezo haya yanazungumzia hali aliyo
nayo Yuda?
B. Soma Mathayo 26:17-22.
Wanafunzi walichukulia kwamba bado
usaliti ulikuwa haujaanza kufanyika. Kwa
nini? (Kwa sababu wote, isipokuwa Yuda,
walikuwa hawajamsaliti Yesu.)
1. Tumejadili mawazo yangu
kuhusu njama ya Yuda. Wanafunzi wengine
walikuwa wanafikiria nini – je, mawazoni
mwao waliwaza kwamba wangeweza
kutengeneza fedha kiasi katika hiki
kizungumkuti cha kubadilika kwa matukio?
(Walikuwa na masikitiko kuhusiana na
habari hii, na walikuwa na wasiwasi
kwamba wanaweza wasiwe watu wa
kutegemewa.)
2. Kwa nini Yesu alibainisha
ukweli kwamba atasalitiwa? Unadhani
alitaka kumfanya Yuda ajisikie hatia, au
alitaka Yuda aachane na mpango wake, au
Yesu alikuwa na wazo jingine mawazoni
mwake?
C. Soma Mathayo 26:23-25. Hili
ni tukio kubwa sana mawazoni mwa
wanafunzi. Je, unadhani walielewa kwamba
Yuda alikuwa anamsaliti Yesu?
1. Ikiwa ndivyo, kwa nini
hawakumshambulia Yuda? Kwa nini
wasimtishe ili asiweze kumsaliti? Kwa nini
wasimzuie (wasimweke kizuizini) ili asiweze
kumsaliti Yesu?
2. Yuda aliposema, “Ni mimi,
Rabi?,” je, hiyo inatuambia nini kuhusu
utayari wake wa kuachana na mpango
wake? (Yuda alikuwa ameshafanya uamuzi.
Sasa alisema uongo ili kuuficha uamuzi
wake.)
III. Mlo Wake wa Mwisho
A. Soma Mathayo 26:26-30. Jiweke
kwenye nafasi ya wanafunzi. Je, ungeweza
kufahamu chochote ya kile ambacho Yesu
alikuwa anakizungumzia? Kwanza anasema
anakaribia kuuawa, na sasa kiishara
anazungumzia kuhusu kuula mwili wake na
kuinywa damu yake.
B. Angalia kile tulichojifunza hadi
sasa. Wanafunzi wanadhani kuwa wana
mawazo mazuri zaidi kuliko ya mwanamke.
Yuda anadhani ana mawazo bora kuliko
mawazo ya Yesu. Unadhani Mathayo
anamaanisha nini kwa kuandika hapa haya
maelezo ya Mlo Wake wa Mwisho?
IV. Petro
A. Soma Mathayo 26:31-35.
Unadhani Petro anasema ukweli? (Soma
Yohana 18:10-11. Katika maelezo ya Yohana
juu ya kukamatwa kwa Yesu, Petro
anachomoa upanga wake, yuko radhi kufa
kwa ajili ya Yesu. Anasema ukweli.)
1. Petro anatofautianaje na
Yohana? (Yesu haenendi ili kujinufaisha
yeye mwenyewe.)
B. Hebu turuke mafungu kadhaa
baada ya kukamatwa kwa Yesu. Soma
Mathayo 26:57-58. Je, bado Petro
anadhihirisha ujasiri mkubwa?
C. Soma Mathayo 26:69-75. Jana,
nilimsikiliza mtu aliyekuwa na dhamira
njema akisimulia jinsi ambavyo tunatakiwa
kutia bidii kujiepusha na dhambi, kwamba
tunakabiliana na Shetani, na kwamba bora
tuwe tayari kwa ajili ya pambano dhidi ya
dhambi (huku Yesu akitusaidia). Anguko la
Petro ni lipi? Anadhihirisha kasoro gani
kitabia? Kuna dosari gani kwenye haiba
yake ni tatizo kubwa? (Petro alikuwa na
Yesu muda wote tena kwa ukamilifu.
Alikuwa radhi kupambana hadi kufa.
Lakini, alichanganyikiwa kwa kitendo cha
Yesu kutopambana na kitendo cha Yesu
kuzungumzia kuhusu kuula mwili wake na
kuinywa damu yake. Yesu hakujua nini cha
kufikiri.)
1. Ni jambo gani basi ambalo
Petro alipaswa kulifanya? (Kumtumaini Yesu
tu.)
D. Hebu turejee kwenye somo
letu. Kwenye mjadala kati ya wanafunzi na
mwanamke juu ya matumizi bora ya
marhamu, nani alikuwa anamtumaini Yesu
na nani alikuwa anayatumaini mawazo yake
mwenyewe? (Wanafunzi walikuwa
wanayatumaini mawazo yao wenyewe.)
E. Katika maelezo ya usaliti wa
Yuda, je, Yuda anamtumaini nani?
(Anajitumainia mwenyewe. Anadhani ana
ufahamu (anajua) zaidi ya Yesu.)
F. Kwenye kumbukumbu ya Mlo
Wake wa Mwisho, Yesu anamaanisha nini
kuhusu kuula mwili wake na kuinywa damu
yake? (Wokovu unapatikana kwa njia ya
Yesu pekee. Yeye ndiye Kondoo wa kafara
wa huduma ya patakatifu (hekalu). Yeye
ndiye njia pekee ya kuufikia wokovu.)
G. Petro hadhani kwamba yeye ni
mwerevu zaidi ya Yesu. Ingawa yu radhi
kufa, kwa namna fulani ameharibu mambo
na kumkana (kumsaliti) Yesu. Je, Petro
alipaswa kufanya nini ili kuepuka matokeo
haya? (Soma tena Mathayo 26:31-33. Petro
angeweka kando majivuno yake na
kumwuliza Yesu, “Nawezaje kuepuka
kufanya hivyo? Niambie ninachotakiwa
kukifanya ili niweze kukusaidia kikamilifu
badala ya kukukana.”)
H. Rafiki, sidhani kama ni wazo
jema kujiandaa kwa ngumi ili kupambana
na Shetani. Sidhani kama ni wazo zuri
kujikita kwenye kuchunguza na kukomesha
kila dhambi maishani mwako. Kiini cha
maisha yako lazima kiwe ni kumtumaini
Mungu, hata pale dunia yote inapoonekana
kuwa nje kabisa ya udhibiti. Unaweza
kuanza kufanya hivyo sasa hivi kwa
kumwomba Roho Mtakatifu kila siku,
kuongoza kila uamuzi wako na kila wazo
lako ili iweze kuwa tabia yako kumtumaini
Mungu.

Jumatano, 22 Juni 2016

Ndoa Ni Ngumu bt ni tamu pia

NDOA SIO UTANI, SOMA STORY HII.

"Mkeo amefariki. Rudi nyumbani kwako haraka sana" Hezron alimwambia Daniel katika simu.

"Mke wangu amekufa? Nini kimetokea? Amekufaje?" Daniel aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa vibaya.

"Daktari amesema ni shinikizo la moyo lililosababishwa na stress kali. Daktari na polisi wapo hapa nyumbani kwako. Njoo haraka" Hezron akaongea kidogo na akakata simu.

Muda anapigiwa simu na Hezron, Daniel alikuwa mtoko na mwanamke mwingine mrembo katika moja ya hoteli kubwa iliyoko maeneo ya Kunduchi. Alikuwa akifurahi nae huku wakinywa vinywaji ghali na chakula cha hadhi ya nyota tano. Lakini baada ya kupokea tu ile simu ya taarifa ya kifo cha mkewe, Daniel alichanganyikiwa, uso wake ukabadilika.

Hezron ni rafiki yake wa karibu.

Daniel akainuka na kuondoka katika ile Hotel akimwacha yule mwanake Mrembo.

"Kuna tatizo gani?" Yule mrembo aliuliza.

"Siwezi kuzungumza" Daniel alijibu na kuondoka haraka.

Daniel akaenda alikopaki gari yake, akaingia, akaiwasha na kukanyaga mafuta, akaiondoa kwa kasi ya ajabu.

Akiwa anaendesha, Daniel akakumbuka jinsi yeye na mkewe anaeambiwa amefariki walivoenda pamoja Showroom ya magari na kununua hilo gari pamoja.

Akiwa anakata kona, akakumbuka jinsi alivyokuwa akimfundisha mkewe kuendesha gari. Hizo zilikua nyakati njema kabisa katika maisha yao ya ndoa.

"Mke wangu amekufa! Kweli mke wangu amekufa! Mungu wangu.." alilia sana huku akiendesha.

Akakumbuka siku ya ndoa yao. Agano waliloliweka pamoja. Akiwa anabadilisha gia, akaangalia vidole vyake asiione pete yake ya ndoa. Pete ya ndoa aliitoa ili kudanganya wanawake wengine kwamba hajaoa.

Daniel akakumbuka ni jinsi gani alivyokuwa akimjibu mkewe hovyo, kwamba anayo kila sababu ya kufurahia maisha na kuponda raha. Akakumbuka maneno ya kuchoma aliyokuwa akimwambia mkewe kwamba yeye amezaa na amezeeka!

"Mke wangu amefariki! Kwanini umefariki Lisa! Kwanini Mungu? Alijiuliza maswali lukuki.

Jibu likamjia. Akakumbuka ni nini Hezron alimwambia. Kwamba mkewe yawezekana amekufa kwa shinikizo la damu kutokana ma stress. Kwa hali hiyo Daniel nimemuua mke wangu.

"Nimemuua mke wangu mwenyewe. Mungu nisamehe..." alijutia huku akiendesha gari kwa kasi.

Daniel akakumbuka jinsi mambo yalivyoenda vibaya katika ndoa yake. Jinsi gani upendo ulikimbia katika ndoa yao. Jinsi gani walivyoanza mabishano na ugomvi. Takribani mara nne ameshampiga mkewe vibao. Alikuwa mtu mbaya kwa mkewe na kwa watoto wake wadogo wawili.

Alifikiri aache kuhudumia familia,  hitaji lake likaja kuwa kutomheshimu mkewe, kutomheshimu mkewe kukaleta dharau na maneno ya kejeli kwa mkewe, maneno ya kejeli yakasababisha vidonda vya tumbo kwa mke mwema Lisa kutokana na mawazo na kutokula.

Naam, Lisa aliugua vidonda vya tumbo kutokana na maumivu ya mawazo aliyosababishiwa na mumewe. Afya yake ilikongoroka, umbo lake zuri namba nane lilipotea, Lisa alionekana kama mzee, wakati ni mwanamke wa miaka 29 tu. Ila Daniel hakujali, alimzarau. Alijibadili kutoka mume aliyempenda mkewe kuwa mtu msaliti, anayemuumiza mkewe. Lisa amefariki!!?

Akiwa bado anaendesha akakumbuka jinsi alivyomfuata Lisa na kumuomba wafunge ndoa, Lisa alikuwa mzuri, akijitegemea na mwenye furaha na maisha. Yeye kumuoa tu ndio ikawa kumharibu, kumuumiza na mwishowe kumuua kwa stress!

Atakufaje? Hawezi kujua kwa sababu hajarudi nyumbani wiki moja sasa imepita, hajui watoto wanakula nini, wanavaa nini. Mke wake alikuwa akimtumia texts na kumpigia akimsisitizia arudi nyumbani, ila kilio cha mkewe kilitua katika masikio yake ambayo hayasikii. Mkewe alikuwa akilia, akipiga kelele mumewe arudi nyumbani, yote hayo ni kwa ajili ya kuokoa ndoa yake. Lakini mimi Daniel sikusikia. Sasa amefariki!

"Mimi nitafanya nini na watoto wangu?" alifikiria nafsini kwake. Watoto wawili alionao ambao alikuwa hawajali kwa sababu ya kuwa busy na warembo wa jiji la Makonda. Akakubali kwamba kweli mke wake alikuwa na moyo wa ajabu, kuwatunza watoto wale wawili bila msaada wake.

"Nani atanisaidia kuwalea? " Wanawake ambao amekuwa akila nao bata hawawezi kumsaidia kulea watoto, sio wife material wale, wife material hawezi kuvunja ndoa ya mwanamke mwenzake. Alifikiria nafsini mwake.

Wazazi wa mkewe watafikiri nini?
Watu watafikiri nini? Mungu ananifikiriaje?
Hii ndio inaishaje ishaje? Ndoa yangu ndio imeishia hivi? Mke wangu kafariki?

Daniel akapaki gari, akatoka na kukimbia ndani ya nyumba.

Akafungua geti, akafungua mlango. Akamuona Hezron, rafiki yake akiwa amesimama katika korido ya nyumba yake.

"Kimetokea nini? Haiwezekani kuwa amekufa. Hawezi kufa. Mimi nitafanya nini Hezron?" Daniel aliongea akiwa amekata tamaa.

Hezron akamkumbatia Daniel.

"Uko sawa Daniel?" Hezron aliuliza.

"Nitakuaje sawa wakati mke wangu amekufa? Mama wa watoto wangu! Uko wapi mwili wake?" Daniel aliuliza.

"Upo sebuleni" Hezron alijibu.

Daniel akakimbia kuelekea sebuleni.

Mshangao!!

Akamwona mkewe akiwa hai. Amekaa katika sofa akiwa na mke wa Hezron ambae ni daktari wa saikolojia pembeni.

"Haujafa?!" Daniel aliuliza akiwa na mshangao

"Ndio hajafariki. Ila kama ukiendelea na hii tabia atafariki siku moja. Mkeo hajawa sawa kabisa. Amekuwa akijaribu kukutafuta na kukurudisha nyumbani ila umempuuza. Taarifa za kifo chake zimekufanya ukimbie kama mwehu. Ulitakiwa ukimbie kwa ajili ya maisha yake na si kwa ajili ya kifo." Mke wa Hezron aliongea.

Daniel akakaa katika kochi mbele ya mkewe na akamshika uso wake. Mkewe akarudishwa kichwa nyuma.

"Natumaini kwamba safari yako ya uchungu kuja hapa ukifikiri mkeo amekufa itakukumbusha ni nini cha muhimu kinachotakiwa kufanywa. Usisubiri mpaka uchelewe ndio ufanye jambo jema. Unayo nafasi ya pili." Aliongea mke wa Hezron

Daniel akanyanyua mkono wa mkewe machozi yakimtiririka, asiamini juu ya kile anachoshuhudia.

"Ndoa sio lelemama nyie wawili. Acheni kucheza michezo ya kipumbavu na maisha. Kesho sio garantii" aliongeza mke wa Hezron.

"Nyie wawili mna matatizo. Mmeridhika na matatizo ya kuumizana hasa wewe shemeji yangu Daniel. Kesho haiwezi kuwa pale kwa ajili yako kwa ajili ya kuomba msamaha. Mkewe Hezron aliongea.

"Na siku ya kiama tutakapokutana na mwenyezi Mungu, Daniel kitu ambacho Mungu atauliza ulimtendaje mke wako ambae ni ubavu wako? Huyu ni binti wa Mungu. Unavomuumiza yeye na Mungu anaumia pia" Akaongezea Hezron.

Mke wa Daniel akamgeukia Hezron na mkewe akasema "Nashukuruni sana kwa kupanga hii idea ya kumuamsha mume wangu, sio siri nilitamani kufa hata leo. Ninampenda sana ila nimechoka na maumivu. Ninyi ni marafiki bora wa familia yetu.

Daniel akamkumbatia mkewe tightly na akasema "Nisamehe sana Lisa wangu, sitaki kukupoteza. Leo nimeshuhudia familia yangu ikivunjika vipande vipande. Nilikuwa kipofu tena katikati ya giza tororo ila sasa ninaona. Usife tafadhali. Nitafanya yale yaliyo bora kuanzia sasa.

Rafiki yangu Hezron na shemeji yangu Julieth ninyi ni marafiki bora kabisa, rafiki aliye bora hukuondoa katika kiza na kukuweka katika nuru. Mmedhihirisha hilo. Naomba niwaahidi tukio hili limekuwa funzo kubwa kwangu. Naanza sasa kuwa mume na baba bora wa familia. Ila siku nyingine msinitishie kifo, naweza kufa kwa pressure na mimi. Nawashukuruni sana. Mwenyezi Mungu awajazi.

"Hahaaa Okey yaishi maneno yako, Mke wangu na mimi tunawaacha, tuwaache mfanye yale ambayo wanandoa wawili wanaopendana kweli hufanya." Hezron aliongea.

Na wakaondoka!
____________________________________________

Mpende mwanandoa mwenzako, waheshimu wazazi, wabariki watoto wako, wapende rafiki zako, wote wakiwa bado wako hai.

Kabla hujachelewa!

Busara yangu, "It's not a lack of love, but a luck of friendship that makes unhappy marriage. Never get tired dating your spouse"

Jumamosi, 18 Juni 2016

Mahubiri ktk kanda ya Kihesa, SDA

PICHA MBALIMBALI ZA MAKAMBI YA UNJILISTI MTAA WA KIHESA http://roryamaendeleo.blogspot.com/2016/06/picha-mbalimbali-za-makambi-ya.html

Jumamosi, 11 Juni 2016

Siku za Mwisho za Yesu

Utangulizi:
Somo letu la Mathayo juma hili
linawamulika wasaliti wawili na mwanamke
mmoja aliyejitoa kikamilifu kwa Yesu. Je,
inamaanisha nini hasa kumsaliti Yesu?
Inamaanisha nini kujitoa kikamilifu kwa
Yesu? Kwa nini matokeo ni tofauti sana kwa
msaliti mmoja kuliko mwingine? Hebu
tuzame kwenye somo letu la Biblia ili
tujifunze zaidi!

I. Wapanga Njama na
Mwanamke
A. Soma Mathayo 26:1-2. Kwa
dhahiri hizi ni habari zenye kukatisha
tamaa sana. Kwa nini uwaambie wanafunzi?
(Yesu alitaka kuwaonya (kwa mara nyingine
tena).)
1. Hiyo inaashiria nini kuhusu
umuhimu wa matukio ya siku za mwisho?
(Yesu atatuonya kuhusu matukio ya
muhimu na yale yenye changamoto.)
B. Soma Mathayo 26:3-7. Tunazo
taswira mbili kinzani. Taswira ya kwanza ni
ya kundi linalopanga kumwua Yesu na
nyingine ni ya mwanamke ambaye anajitoa
kwa hali ya juu kwa ajili ya Yesu. Kutokana
na Yesu kuelewa mustakabali wa mauti
yanayomkabili kitambo kifupi kijacho,
unadhani alijisikiaje kuhusu huyu
mwanamke? (Hii ni nyota inayong’aa
kwenye mazingira ya giza. Ningemshukuru
sana mwanamke huyu.)
C. Soma Mathayo 26:8-9.
Unauelezeaje mwitiko wa wanafunzi?
Wameambiwa kwamba Yesu anakaribia
kufa, je, hawapaswi kushiriki katika
kumfanyia jambo la pekee? (Nadhani
wanafunzi walipingana na uhalisia kwa
kutokubali kuamini kile alichowaambia
Yesu. Hawakutaka kuamini kuwa atakufa.)
1. Je, ungekuwa na mwitiko gani
endapo wewe ndiye ungekuwa huyu
mwanamke na kusikia ukosoaji huu?
Umejitoa kwa kununua hii marhamu, na
sasa wanafunzi wanakukosoa!
2. Kuna dhana katika fungu hili
ambayo nataka uiangalie. Wanafunzi
hawakusema kwamba mwanamke alipaswa
kutoa fedha kwa masikini badala ya
kununua marhamu, bali walisema kuwa
angeweza kuiuza hiyo marhamu. Hii
inatuambia nini kuhusu jinsi mwanamke
huyu alivyoipata hii marhamu? (Ilikuwa ni
zawadi. Kwa uthibitisho, hakikuwa kitu
ambacho angeweza kumudu kukinunua.)
D. Soma Mathayo 26:10-13. Hii
ilikuwa ni zawadi, kuna mtu alidhamiria
mwanamke huyu aweze kuitumia zawadi
hiyo. Badala yake, alichagua kujikana nafsi
kwa kutoitumia kama walivyopendekeza
wanafunzi. Je, wanafunzi walikuwa na haki
ya kumwambia kufanya matumizi
anayopaswa kujikana nafsi ili kutoyafanya?
(Hawana ushauri sahihi. Yesu anasema
kuwa alichokifanya mwanamke huyu
kitaongelewa katika kumbukumbu lake na
historia yote.)
1. Je, zipo fursa
zinazokuzunguka kuinua mioyo ya watu
waliokata tamaa kwa kuwatendea wema?
2. Je, pia watazungumzia
duniani kote kuhusu habari ya wanafunzi
kumkosoa mwanamke huyu aliyejikana
nafsi?
3. Kuna tofauti gani kati ya
mtazamo wa mwanamke na ule wa
wanafunzi? (Alikuwa amejitoa kwa Yesu
kikamilifu. Wanafunzi walijitoa kufanya
uamuzi wa matumizi bora ya marhamu
yake.)
II. Yuda
A. Soma Mathayo 26:14-16. Je,
Yuda ndiye aliyemkosoa mwanamke?
1. Unadhani kwa nini Yuda
alimsaliti Yesu? Je, sasa aliamua kumchukia
Yesu? (Ninazo nadharia mbili. Kwanza,
hakuamini kwamba Yesu angeweza kuuawa
– na kwamba angeweza pia kupokea fedha
kama thawabu kwa kumlazimisha Yesu
kujitangaza kuwa Mfalme. Pili, kwamba
Yesu alimaanisha sana juu ya kifo chake,
kiasi kwamba alistahili fedha kwa muda
alioupoteza kwa kuzunguka kwake kote kwa
muda wa miaka mitatu. Katika nadharia
zote mbili, alijitumainia yeye mwenyewe na
wala hakumtumaini Yesu.)
2. Soma Mathayo 18:7. Je,
maelezo haya yanazungumzia hali aliyo
nayo Yuda?
B. Soma Mathayo 26:17-22.
Wanafunzi walichukulia kwamba bado
usaliti ulikuwa haujaanza kufanyika. Kwa
nini? (Kwa sababu wote, isipokuwa Yuda,
walikuwa hawajamsaliti Yesu.)
1. Tumejadili mawazo yangu
kuhusu njama ya Yuda. Wanafunzi wengine
walikuwa wanafikiria nini – je, mawazoni
mwao waliwaza kwamba wangeweza
kutengeneza fedha kiasi katika hiki
kizungumkuti cha kubadilika kwa matukio?
(Walikuwa na masikitiko kuhusiana na
habari hii, na walikuwa na wasiwasi
kwamba wanaweza wasiwe watu wa
kutegemewa.)
2. Kwa nini Yesu alibainisha
ukweli kwamba atasalitiwa? Unadhani
alitaka kumfanya Yuda ajisikie hatia, au
alitaka Yuda aachane na mpango wake, au
Yesu alikuwa na wazo jingine mawazoni
mwake?
C. Soma Mathayo 26:23-25. Hili
ni tukio kubwa sana mawazoni mwa
wanafunzi. Je, unadhani walielewa kwamba
Yuda alikuwa anamsaliti Yesu?
1. Ikiwa ndivyo, kwa nini
hawakumshambulia Yuda? Kwa nini
wasimtishe ili asiweze kumsaliti? Kwa nini
wasimzuie (wasimweke kizuizini) ili asiweze
kumsaliti Yesu?
2. Yuda aliposema, “Ni mimi,
Rabi?,” je, hiyo inatuambia nini kuhusu
utayari wake wa kuachana na mpango
wake? (Yuda alikuwa ameshafanya uamuzi.
Sasa alisema uongo ili kuuficha uamuzi
wake.)
III. Mlo Wake wa Mwisho
A. Soma Mathayo 26:26-30. Jiweke
kwenye nafasi ya wanafunzi. Je, ungeweza
kufahamu chochote ya kile ambacho Yesu
alikuwa anakizungumzia? Kwanza anasema
anakaribia kuuawa, na sasa kiishara
anazungumzia kuhusu kuula mwili wake na
kuinywa damu yake.
B. Angalia kile tulichojifunza hadi
sasa. Wanafunzi wanadhani kuwa wana
mawazo mazuri zaidi kuliko ya mwanamke.
Yuda anadhani ana mawazo bora kuliko
mawazo ya Yesu. Unadhani Mathayo
anamaanisha nini kwa kuandika hapa haya
maelezo ya Mlo Wake wa Mwisho?
IV. Petro
A. Soma Mathayo 26:31-35.
Unadhani Petro anasema ukweli? (Soma
Yohana 18:10-11. Katika maelezo ya Yohana
juu ya kukamatwa kwa Yesu, Petro
anachomoa upanga wake, yuko radhi kufa
kwa ajili ya Yesu. Anasema ukweli.)
1. Petro anatofautianaje na
Yohana? (Yesu haenendi ili kujinufaisha
yeye mwenyewe.)
B. Hebu turuke mafungu kadhaa
baada ya kukamatwa kwa Yesu. Soma
Mathayo 26:57-58. Je, bado Petro
anadhihirisha ujasiri mkubwa?
C. Soma Mathayo 26:69-75. Jana,
nilimsikiliza mtu aliyekuwa na dhamira
njema akisimulia jinsi ambavyo tunatakiwa
kutia bidii kujiepusha na dhambi, kwamba
tunakabiliana na Shetani, na kwamba bora
tuwe tayari kwa ajili ya pambano dhidi ya
dhambi (huku Yesu akitusaidia). Anguko la
Petro ni lipi? Anadhihirisha kasoro gani
kitabia? Kuna dosari gani kwenye haiba
yake ni tatizo kubwa? (Petro alikuwa na
Yesu muda wote tena kwa ukamilifu.
Alikuwa radhi kupambana hadi kufa.
Lakini, alichanganyikiwa kwa kitendo cha
Yesu kutopambana na kitendo cha Yesu
kuzungumzia kuhusu kuula mwili wake na
kuinywa damu yake. Yesu hakujua nini cha
kufikiri.)
1. Ni jambo gani basi ambalo
Petro alipaswa kulifanya? (Kumtumaini Yesu
tu.)
D. Hebu turejee kwenye somo
letu. Kwenye mjadala kati ya wanafunzi na
mwanamke juu ya matumizi bora ya
marhamu, nani alikuwa anamtumaini Yesu
na nani alikuwa anayatumaini mawazo yake
mwenyewe? (Wanafunzi walikuwa
wanayatumaini mawazo yao wenyewe.)
E. Katika maelezo ya usaliti wa
Yuda, je, Yuda anamtumaini nani?
(Anajitumainia mwenyewe. Anadhani ana
ufahamu (anajua) zaidi ya Yesu.)
F. Kwenye kumbukumbu ya Mlo
Wake wa Mwisho, Yesu anamaanisha nini
kuhusu kuula mwili wake na kuinywa damu
yake? (Wokovu unapatikana kwa njia ya
Yesu pekee. Yeye ndiye Kondoo wa kafara
wa huduma ya patakatifu (hekalu). Yeye
ndiye njia pekee ya kuufikia wokovu.)
G. Petro hadhani kwamba yeye ni
mwerevu zaidi ya Yesu. Ingawa yu radhi
kufa, kwa namna fulani ameharibu mambo
na kumkana (kumsaliti) Yesu. Je, Petro
alipaswa kufanya nini ili kuepuka matokeo
haya? (Soma tena Mathayo 26:31-33. Petro
angeweka kando majivuno yake na
kumwuliza Yesu, “Nawezaje kuepuka
kufanya hivyo? Niambie ninachotakiwa
kukifanya ili niweze kukusaidia kikamilifu
badala ya kukukana.”)
H. Rafiki, sidhani kama ni wazo
jema kujiandaa kwa ngumi ili kupambana
na Shetani. Sidhani kama ni wazo zuri
kujikita kwenye kuchunguza na kukomesha
kila dhambi maishani mwako. Kiini cha
maisha yako lazima kiwe ni kumtumaini
Mungu, hata pale dunia yote inapoonekana
kuwa nje kabisa ya udhibiti. Unaweza
kuanza kufanya hivyo sasa hivi kwa
kumwomba Roho Mtakatifu kila siku,
kuongoza kila uamuzi wako na kila wazo
lako ili iweze kuwa tabia yako kumtumaini
Mungu.

Jumapili, 5 Juni 2016

Matukio ya Siku za Mwisho.

(Mathayo 23 & 24)

Utangulizi:
Mojawapo ya faida maridhawa
ya kuandika masomo haya ni kwamba
yananilazimisha kujifunza Biblia. Malengo
makuu ya kuandika masomo haya ni
kuiboresha Shule ya Sabato na kuwasaidia
wanafunzi kuyaelewa mapenzi ya Mungu
vizuri zaidi. Hata hivyo, ninapojifunza Biblia
mara zote huwa ninafikiria juu ya athari za
neno la Mungu maishani mwangu. Juma hili
baadhi ya kauli za Mathayo zinaingiliana
sana na maisha yangu binafsi kiasi kwamba
natangulia kuomba radhi kwa kujihusisha
sana katika somo hili. Hebu tuchimbue zaidi
na tuone kama wewe pia unajisikia
kujihusisha na somo letu la Biblia!

I. Walafi wa Sifa
A. Soma Mathayo 23:1-4.
Unapotambua kwamba mtu fulani ni
mnafiki, je, unayachukuliaje mafundisho ya
mtu huyo? (Wazo la jumla ni kuyakataa
mafundisho ya mtu mnafiki.)

1. Kwa nini Yesu anasema kuwa
wanafiki hawa waheshimiwe? (Kwa sababu
“wanaketi katika kiti cha Musa.”)
a. Hiyo inamaanisha nini, na
kwa nini jambo hilo ni muhimu sana?
(Nadhani inamaanisha kwamba
wanafundisha torati iliyotolewa na Mungu
kupitia kwa Musa.)

2. Nawakumbuka viongozi wa
dini kadhaa maarufu waliokuwa na dhambi
maarufu. Mwitiko wangu ulikuwa ni
kwamba waliikumbatia na kuikubali dhambi
– jambo ambalo ni kweli kwetu sote.
Tunawezaje kuwatofautisha wale viongozi
wa dini “walioketi katika kiti cha Musa” na
wale wanaotupotosha? (Sababu kuu ya
kuanza na maswali yanayotokana na fungu
la Biblia katika mfululizo wa masomo haya
ni kwamba hatuwezi (natumaini hivyo)
kupotoka sana ikiwa tutajikita kwenye neno
la Mungu. Suala la muhimu zaidi ni endapo
kiongozi anafundisha Biblia au anafundisha
kitu kingine kabisa.)

B. Soma Mathayo 23:5-7. Kuwa
mwaminifu. Je, unapenda kutukuzwa,
pamoja na kupewa kiti bora kabisa? Je,
unapenda kusalimiwa na watu
wanaokuheshimu? (Ikiwa umesema
“hapana,” nadhani tu kwamba umevunja
Amri ya Tisa. Sote tunapenda kutukuzwa/
kuheshimiwa.)
1. Tunawezaje kuepuka kuwa
kama hawa viongozi wa dini? (Angalia tena
fungu la 5, “matendo yao yote huyatenda ili
kutazamwa na watu.” Ikiwa kila jambo
unalolitenda linahamasishwa na kujitukuza
kwako, tofauti na kumpa Mungu utukufu au
kumpenda mtu mwingine, basi una tatizo
kubwa.)

C. Soma Mathayo 6:2. Nini
maana ya “wamekwisha kupata thawabu
yao?” Je, inamaanisha kwamba “thawabu
kamili” ni kujitukuza binafsi –
itakayokukosesha mbingu? (Napenda
kuhubiri, ninapenda kufundisha, na hakuna
shaka yoyote kwamba sehemu ya sababu
yangu ni kwamba ninataka watu wamjue
Mungu vizuri zaidi. Lakini, sehemu nyingine
ya sababu zangu ni kwamba ninapenda
watu waseme kuwa, “anafanya kazi nzuri.”
Ninaposoma habari za hawa viongozi wa
dini ambao thawabu yao pekee ipo hapa,
ninasikitika. Dkt. William H. Shea ni
mmojawapo wa Wakristo wa pekee kabisa
niliowahi kuwafahamu. Ni mwerevu sana
na mnyenyekevu kupindukia. Nilimuuliza,
“Je, unafurahia heshima/sifa unayopewa
kwa kuhubiri na kufundisha?” Alijibu,
“ndiyo,” hiyo ni sehemu mojawapo. Hiyo
iliufanya moyo wangu utulie katika suala
hili.)

D. Soma Mathayo 23:8-12.
Mmojawapo wa wanafunzi wangu wa
zamani alikuwa akiniita “rabi” na mara kwa
mara mke wangu huniita “profesa.”
Wanangu wananiita “Baba.” Wanafunzi
katika shule ya sheria huniita “Profesa
Cameron.” Je, ninapaswa kuwaambia wote
hawa waache kuniita hivyo?

1. Soma Kutoka 20:12. Suala
mojawapo ni kuwaheshimu viongozi wa
dini. Fungu hili linatuambia tuwaheshimu
wazazi wetu – na hiyo inajumuisha kumuita
baba yangu kuwa “Baba.” Unawezaje
kuelewa mkanganyiko wa dhahiri uliopo
kwenye Biblia?

2. Kumbuka muktadha. Je,
viongozi wa dini wananyakua heshima gani
isivyostahili? (Wanadai heshima
inayomstahili Mungu. Wanafanya kila jambo
kwa ajili ya utukufu wao, na sio utukufu wa
Mungu au upendo kwa watu wengine.
Utagundua kwamba katika Mathayo 23:8-10
anayepaswa kurelejewa ni Mungu.
Wanangu, mke wangu, wanafunzi wangu
hawadhani kwamba mimi ni Mungu na
sijaribu kuwachanganya akili katika jambo
hilo.)

E. Hebu turuke mafungu kadhaa
hadi Mathayo 23:37-39. Tatizo la msingi la
viongozi wa dini Yerusalemu lilikuwa ni
lipi? (Walimkataa Yesu. Utaona kwamba
mjadala wa “mada” ni sehemu ya kumkataa
Yesu. Sasa Yesu anasema kuwa mwisho wao
umefika. Hawako radhi kumkubali au
kumpa utukufu.)

II. Kubomolewa

A. Soma Mathayo 24:1. Unadhani
kwa nini wanafunzi walimwambia Yesu
aangalie majengo ya hekalu? (Pasi na shaka
majengo hayo yalikuwa mazuri. Nimesoma
maelezo ya Josephus kuhusu hekalu na
maelezo hayo yalikuwa mazuri ajabu.)

B. Soma Mathayo 24:2-3. Bila
shaka habari hii ni ya kutisha. Kwa nini
wanafunzi walimwendea Yesu kwa
“faragha” ili kutaka kufahamu habari kwa
kina zaidi?

1. Unaona maswali mangapi
katika mafungu haya? Unadhani wanafunzi
walidhani walikuwa wanamuuliza Yesu
maswali mangapi? (Nadhani walikuwa
wanauliza angalao maswali mawili, lakini
nadhani walidhani kwamba walikuwa
wanauliza swali moja tu. Bila shaka
walidhani kuwa hekalu halitabomoshwa
hadi Yesu atakaporejea “mwisho wa
dahari.”)

III. Mwisho

A. Soma Mathayo 24:4. Yesu
anajali jambo gani kwanza? (Kwamba
tuepuke kudanganywa/kulaghaiwa.)

B. Soma Mathayo 24:5-14. Mara
tatu Yesu anarejea “nyakati za mwisho”
katika hivi vifungu. Anajadili mwisho gani,
mwisho wa hekalu au mwisho wa dunia?

C. Soma Mathayo 24:15-20.
Unadhani jambo gani linajadiliwa hapa? (Ni
kawaida kwamba unabii unaweza
kutimizwa zaidi ya mara moja. Lakini hii
inaonekana kuendana na kubomolewa kwa
Israeli. Wakristo wengi waliukimbia mji na
waliokolewa kabla ya hekalu kuangamizwa
na Warumi.)

D. Soma Mathayo 24:23-27. Jambo
gani linaelezewa hapa? (Ujio wa Yesu Mara
ya Pili.)

1. Kuna jambo gani mahsusi
kuhusu Wakristo kudanganywa? (Watatokea
makristo wa uongo – na ishara zao na
miujiza yao ina ushawishi mkubwa sana.)

2. Tunawezaje kuepuka
kudanganywa? (Hakuna mtu atakayetakiwa
kutuambia kuhusu ujio wa Yesu Mara ya
Pili. Watu wote watauona kwa mara moja.
Nimeepuka baadhi ya masuala magumu
zaidi kwenye ujumbe wa Yesu kwa sababu
ninaweza kukosea. Hata hivyo, sehemu
rahisi ya ujumbe huo iko dhahiri kabisa –
utafahamu tu Yesu atakapokuja!)
a. Kwa nini basi Yesu anatuonya
kwamba tunatakiwa kuepuka kudanganywa,
na kwamba uongo ujao utakuwa na nguvu
kubwa sana? (Tuna nafasi kubwa sana ya
kudanganywa na hao walaghai. Ikiwa
unajihusisha kwenye mjadala unaomhusisha
mtu fulani kwamba ni Yesu, basi huo ni
uthibitisho madhubuti kwamba mtu ni
mlaghai na si Yesu!)

E. Soma Mathayo 24:30-31 na
Mathayo 24:40-41. Je, tutakuwa na
uthibitisho gani mwingine kamili kuhusu
ujio wa Yesu Mara ya Pili? (Watakaookolewa
watachukuliwa mbinguni!)

1. Je, “sauti ya parapanda”
inahusu nini? (Soma 1 Wakorintho 15:51-52.
Wale waliokufa wakimtumaini Yesu
watafufuliwa kwa dakika moja, kufumba na
kufumbua wakati wa mlio wa parapanda.)

F. Hebu tupitie mambo yote
haya ili usiweze kudanganywa. Jambo gani
litatokea Yesu atakapokuja tena? (Mwanga
kama wa radi utatokea duniani kote – kila
mtu atauona kwa wakati mmoja. Waliokufa
katika Kristo watafufuliwa kutoka
makaburini. Watakaookolewa wakiwa hai
watakuchukuliwa mbinguni.
Hautachanganyikiwa kuhusiana na hili
tukio. Ikiwa hutachukuliwa mbinguni, hiyo
ni habari mbaya sana.)

G. Soma Mathayo 24:42-44. Hebu
subiri kidogo, hivi punde tu tumejifunza
kwamba ujio wa Yesu Mara ya Pili utakuwa
dhahiri kwa kila mtu. Kwa nini tunaonywa
“kukesha” na kuhusu matatizo ya ujio wa
ghafula? Ninaweza kuwa kwenye usingizi
mzito lakini sitaweza kuukosa ujio wa Yesu
Mara ya Pili! (Mwizi havunji na kuingia
nyumbani kwa Yesu katika huu mfano.
Mwizi anavunja na kuingia nyumbani
kwako. Onyo halihusu utata juu ya ujio wa
Yesu, bali endapo u tayari!)

H. Soma Mathayo 24:45-46.
Unapaswa kuwa unafanya nini wakati
ukiutarajia ujio wa Yesu Mara ya Pili? (Kazi
yako – “kuwalisha” watumishi wa Yesu.
Tunatakiwa kuendelea kufanya kazi ili
kuuendeleza Ufalme wa Mungu!)

I. Rafiki, viongozi wa dini
walikuwa na tatizo gani tulilolijadili
mwanzoni mwa somo hili? Tatizo ni
kwamba walikuwa wanafanya kazi ya
kuuendeleza utukufu wao wenyewe. Yesu
anatupatia wito wa kufanya nini wakati
tunasubiria kurudi kwake? Kuuendeleza
Ufalme wa Mungu. Je, unafanya nini siku
hizi? Je, unauendeleza utukufu wako au
Ufalme wa Mungu? Ikiwa hulipendi jibu
lako, kwa nini usitubu sasa hivi na
umwombe Roho Mtakatifu akuoneshe njia
bora zaidi?

IV. Juma lijalo: Siku za Mwisho za
Yesu.