Jumatano, 6 Julai 2016

LESSON J5: TAR; 6/7/2016 UTUNZAJI WA DUNIA

Somo; UTUNZAJI WA DUNIA

"Bwana Mungu akamtwaa huyo  mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime  na kuitunza." (Mwanzo 2:15). Ni kanuni zipi, kama zipo, tunazoweza kuchukua katika aya  hii ambazo  zitaathiri namna tunavyohusiana na sayari yetu kwa vigezo vya kuitunza?

Kabla ya dhambi, Adamu na Hawa walikuwa wamefanywa kuwa mawakili juu ya vyote ambavyo  Mungu alikuwa amewakabidhi. Walikuwa wamepewa uwezo kamili juu ya maisha ya mimea  na wanyama. Baada ya dhambi, hata hivyo, viumbe vyote vya asili vilionekana kuasi dhidi yao  kwa kiwango kile  kile  walichokuwa wameasi dhidi ya Mungu. Wanadamu wakaanza kujiona kutokuwa  na uwezo mbele ya vitu vya asili ( kama vile hali ya hewa, kilimo na jamii ya wanyama.)

" Miongoni mwa wanyama wengine wakawaida, Adamu alikuwa amesimama kama mfalme, lakin kama angebakia kuwa mwaminifu kwa Mungu, viumbe vyote vya asili vingeendelea kuutambua utawala wake; bali  alipoasi, mamlaka haya yalipotea. Roho ya uasi aliyokuwa  ameiruhusu mwenyewe kuingia ilisambaa pia kwa wanyama wengine. Kwa namna hiyo, sio tu maisha ya mwanadamu, yaliyokuwa yanasimulia kisa  cha huzuni cha somo  la  ujuzi wa  uovu, Bali pia hali ya asili ya wanyama, miti ya misituni, nyasi za uwandani, na hata hewa yenyewe aliyokuwa  anavuta, vyote vilisimulia somo la  kuhuzunisha la  ujuzi Wa mabaya." Ellen G. White, Education, uk. 26,27.

Mpaka sasa, bado tunasumbuliwa na kuteketezwa na majanga ya asili pamoja na mfumo wa  ekolojia unaochakaa kila  leo, yumkini katika baadhi ya maeneo duniani. Na kwa hiyo, tunatumia juhudi nyingi za kutumia  teknolojia na maendeleo ya viwanda kujihami. Hata hivyo, ingawa teknolojia na maendeleo ya viwanda yanaweza kutusaidia kujikinga, wakati mwingine teknolojia hiyo hiyo inaweza  kuiharibu sayari yetu. Ekolojia ni suala mtambuko linalohusika  kimafundisho, kimaadili, na kiteolojia, hasa  pale ambapo matumizi ya rasilimali zilizomo duniani  kunaweza kuwaweka watu wengine kwenye hali ngumu kupindukia.

"Waadventista Wa sabato hutetea mtindo Wa maisha ulio sahili na wenye  kuleta siha kamili, mahali ambapo watu hawarukii kwenye gurudumu LA kuendesha mashine  isiyodhibitiwa ya ufujaji, kunipatia vitu na  uzalishaji Wa taka. Tunawataka watu waheshimu viumbe vya Mungu, kujizuia katika matumizi ya rasilimali zilizomo duniani, kutathmini upya mahitaji  ya kila  mmoja wetu, na kutilia mkazo kuheshimu viumbe wengine."- kutoka katika "Official Statement of the Seventh - day Adventist Church on Environment, [Tamko Rasmi la  kabisa la  Waadventista Wa Sabato kuhusu mazingira]" 1995.

Tunafikiaje mapatano ya haki katika mtazamo wetu  juu ya dunia: kuwa mawakili wema  Wa makao tuliyopewa na wakati huo  huo  tukijiepusha na hatari ya kuifanya  dunia na mazingira kuwa miungu tunayoiabudu? Warumi 1:25 hapa ina  onyo gani kwetu?
➖➖➖➖➖➖➖➖➖
MWISHO WA NUKUU

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni